Habari kuhusu Kiingereza kutoka Agosti, 2010
Tunisia: Picha ‘Zilizochakachuliwa’ ni Dalili ya Hali Halisi katika Vyombo vya Habari vya Kitaifa
Utumiaji vyombo vya habari vya kitaifa nchini Tunisia kama chombo vya kupigia propaganda ni jambo ambalo limeripotiwa vya kutosha. Ushahidi wa hivi karibuni kabisa wa utumiaji mbaya wa vyombo vya habari umewekwa bayana na wanablogu wa nchi hiyo mnamo tarehe 20 Agosti baada ya magazeti ya Le Temps na Assabah kuchapisha ripoti kuhusu taasisi ya hisani ya Zeitouna kutuma msaada wa kibinadamu wa chakula kwa waathirika wa mafuriko nchini Pakistani.
Malaysia: Je, Uhuru wa Habari Unaelekea Wapi Sasa?
Picha uliyonayo ni kwamba Malaysia inaweza kuwa ni moja ya nchi zinazokua haraka kiuchumi katika bara la Asia, lakini je unafahamu kuwa ilikuwa katika nchi tatu za mwisho (nchi ya 131) kwenye masuala ya uhuru wa vyombo vya habari? Je wananchi na vyama vya upinzani vinavyopigana dhidi ya uchujwaji wa habari wanapata ahueni? Tutajua ukweli kwa kuangalia hali ya sasa ya uhuru wa vyombo vya habari nchini Malaysia.
Jamaica: Dansi!
Tallawah ametuma picha kutoka katika muhula wa 2010 wa Kikundi cha Taifa cha Dansi cha Jamaica.
China: Pato la Taifa Linaongezeka, Matumizi Katika Huduma za Jamii je?
Tunaendelea kusikia kuwa uchumi wa China unaendelea kukua; je matumizi ya huduma za jamii yameongezeka? Akiba binafsi zinabaki kwenye benki, anaandika mwanablogu mmoja: kutokea hospitali mpaka shuleni mpaka malipo ya uzeeni, China haiwezi kujilinganisha.
Mashindano ya Video: Intaneti Kama Chombo cha Kueneza Amani
Mfumo wa Intaneti umependekezwa kwa ajili ya kupata Tuzo ya Amani ya Nobel kwa mwaka 2010. Kama sehemu ya mjadala unaoendelea kuhusu mchango wa Intaneti katika jamii nzima ya binadamu , Condé Nast na Google Ireland wameungana na kuandaa mashindano haya ya video na mshindi atapata fursa ya kusafiri na pia video yao kuoneshwa kupitia MTV ya Italia.
Ufilipino: Maoni ya Wanablog Juu ya Elimu ya Ya afya ya Uzazi
Mwaka huu wa masomo serikali ya Philippines inatekeleza mpango wa elimu ya uzazi kwenye shule za umma unaofadhiliwa na Umoja wa Mataifa kwa ajili ya watoto na vijana. Na wanablogu wametoa maoni juu ya suala hilo.
Afrika Kusini: Wanablogu Wajadili Hukumu ya Mkuu wa Zamani wa Jeshi la Polisi
Siku ya ijumaa tarehe 2 Julai 2010, aliyekuwa mkuu wa polisi na rais wa zamani wa Shirika la Kimataifa la Polisi (Interpol) Jack Selebi alihukumiwa kwa kosa la rushwa. Hukumu hiyo imezua mdahalo nchini na kadhalika imeacha maswali mengi yasiyo na majibu.
Udhibiti Nchini Singapore
Singapore imesababisha kelele kubwa baada ya kupiga marufuku filamu ya aliyewahi kuwa mfungwa wa kisiasa na kumkamata mtunzi Mwingereza wa kitabu kilichoandiaka kuhusu adhabu ya kifo nchini humo. Wanablogu wanajadili.