Habari kuhusu Kiingereza kutoka Julai, 2012
Basi la Watalii Raia wa Israeli Lashambuliwa Nchini Bulgaria
Watu wapatao saba wameuawa katika shambulio la la kijana wa Kiyahudi katika basi la kitalii lililokuwa katika uwanja wa ndege wa Burgus nchini Bulgaria. Ripoti zinadai shambulio linaonekana kuwa la kujitolea mhanga, lililofanywa na kijana alikuwa ama karibu na basi au alikuwa ndani ya basi.
Afrika: Usanii wa Kisasa wa ki-Afrika Mtandaoni
Usanii Afrika blogu inayoonyesha usanii wa kisasa wa ki-Afrika: Usanii Afrika ni blogu iliyozaliwa kutokana na upenzi. Akiwa amezaliwa na kipaji cha ubunifu yeye mwenyewe, mwanablogu, Kirsty Macdonald amekuwa na mahusiano ya karibu na masuala ya sanaa na kujieleza”
Ethiopia: Maandamano ya Waislamu Yashika Kasi
Jeshi la Polisi nchini Ethiopia waliamua kutumia nguvu kupambana na wanaharakati wa ki-Islamu, likituhumiwa kufanya vitendo haramu katika maeneo yanayochukuliwa kuwa matakatifu katika misikiti, kwa mujibu wa habari zilizoandikwa na ukurasa wa kikundi cha waislam katika mtandao wa Facebook uitwao Dimtsachin Yisema (Iache Sauti Yetu Isikike). Tangu mwezi Mei, Wa-Islamu wa ki-Ethiopia wamekuwa wakiandamana kupinga serikali kuingilia mambo yao ya kidini.
Afghanistan: Mwanafunzi wa Sekondari Agundua Kanuni ya Hisabati
Mwanafunzi wa Sekondari nchini Afghanistan amegundua kanuni ya kimahesabu inayoweza kutumika kukokotoa milinganyo ya kwadratiki. Watumiaji wa twita wamezipokea habari hizo kama ishara ya maendeleo ya sekta ya elimu nchini humo.
Afrika: Ujuzi wa Matumizi ya Zana za Habari za Kijamii kwa Vijana Wanaoishi na Ulemavu.
Warsha ya vijana walemavu kutoka kote barani Afrika lafanyika Dakar, Senegali. Warsha hii ilipangwa na DRI na YI. Imeandikiwa na Haute Haiku.
Uganda: Aina Mpya ya Kifafa Yatishia Maisha ya Watoto.
James Propa shares photos and YouTube videos of the effects of nodding disease in Uganda. Nodding disease is a mentally and physically disabling disease that mostly affects children. It is currently restricted to small regions in South Sudan, Tanzania and northern Uganda.
Wananchi wa Mexico Wanamchagua Rais Mpya
Mnamo tarehe 1 Julai, Wa-Mexico walipiga kura kumchagua rais wao mpya. Punde tu kura zilipoanza kupigwa, watumiaji wa mtandao wa intaneti walianza kutoa mawazo na uzoefu wao. Walipanga pia namna tovuti na alama ishara za mtandao wa twita zitakavyotumika kukusanya taarifa juu ya udanganyifu na nyendo zilizo kinyume cha sheria wakati wa uchaguzi huo.
Palestina: Makala Kuhusu Kifo cha Arafat yaibua maswali
Kituo cha habari cha Al Jazeera hivi karibuni kilionyesha makala iliyohusu kifo cha utata cha rais wa Palestina Yasser Arafat kilichotokea mjini Paris mnamo Novemba, 2004. Makala hayo yanadai kwamba kiongozi huyo hakufa kifo cha kawaida, ila aliwekewa sumu ya poloni, madai ambayo yanaibua maswali mengi.
Uganda: Kuvunja Utamaduni wa Ukimya Kuhusu Haki za Afya.
A video produced by Results for Development, an international non-profit organisation whose mission is to unlock solutions to tough development challenges, was released online recently to encourage Ugandans to break the culture of silence and take control of their health rights.A video produced by Results for Development, an international non-profit organisation whose mission is to unlock solutions to tough development challenges, was released online recently to encourage Ugandans to break the culture of silence and take control of their health rights.
Somalia: Migawanyiko Mikubwa Kuhusu Katiba Mpya
Somalia, ambayo haijawahi kuwa na serikali kuu inayotawala nchi nzima tangu mwaka 1991, inaandika rasimu ya katiba mpya ambayo inatarajiwa kuhitimisha muda wa utawala wa serikali ya mpito iliyopo madarakani na kumchagua rais mpya. Hapa tumekusanya mijadala na mazungumzo ynayoendelea mtandaoni kuhusu rasimu hiyo ya katiba.