Habari kuhusu Kiingereza kutoka Agosti, 2012
Nigeria: Rais wa Seneti Atakiwa Kuwataja Wafadhili wa Boko Haram
Makundi mawili ya vijana Kaskazini mwa Nigeria Jumatano yalimkosoa Rais wa Seneti, David Mark, kutokana na matamshi aliyotoa siku za karibuni akiwataka viongozi wa mikoa ya kaskazini kudhibiti shughuli za kundi linaloogopwa sana la Boko Haram, Connected Africa anaripoti.
Kocha wa Timu ya Taifa ya Zambia Atunukiwa Ukaazi wa Kudumu
Zambia imewahi kuwa na makocha wengi wa kigeni wa timu ya Taifa ya soka, lakini ni Mfaransa Herve Renard, aliyeongoza timu hiyo hadi kushina Kombe la Washindi Barani Afrika mwaka 2012, aliyepata upendeleo wa pekee. Ili kutambua mafanikio yake haya, serikali imemtunuku ukaazi wa kudumu lakini uamuzi huo unaonekana kuwekewa chumvi ya kisiasa.
Tanzania/Malawi: Utafutaji Mafuta kwenye Ziwa Nyasa WachocheaMgogoro wa Umiliki
Taarifa kwamba Malawi inatafiti mafuta katika Ziwa Nyasa (linalojulilkana pia kama Ziwa Malawi) zimeibua mjadala motomoto. Wakati ambapo serikali ya Malawi inadai umiliki kamili wa ziwa hilo, Tanzania inataka mpaka utambuliwe kuwa katikati ya ziwa.
Sudani: Mwanaharakati Mtumia Twita Aachiwa Huru
'Nilitishiwa kufanyiwa vitendo vya ngono na kutendewa vibaya mara kadhaa katika siku ile. Wakati mmoja hata na ofisa wa ngazi za juu wa #NISS.' Mwezi Juni, Shirika la Ujasusi na Usalama wa Taifa la Sudani liliwakamata maelfu ikiwa ni pamoja na mwanaharakati anayetumia Twita Usamah Mohamed Ali.
Mgogoro wa Umoja wa Ulaya: Kitabu cha Kwanza cha Global Voices cha Kieletroni
"Umoja wa Ulaya katika Mgogoro" (EU in Crisis) ni chapisho letu la kwanza katika Mradi wa Vitabu wa Global Voices na ambao unahusisha makala bora zaidi kuhusu mazungumzo ya kijamii, ushiriki na uhamasishaji unaopewa nguvu na raia wanaopitia nyakati ngumu za kubana matumizi katika bara la kale zaidi na kwingineko.
Mfumo wa Kipekee wa Kuwapa watoto Majina wa Nchini Myanmar (Burma).
Raia wengi wa Myanmar hawana majina ya ukoo. Je, umewahi kujiuliza wanajaza vipi fomu zinazowadai kujaza majina yao ya mwanzo na ya ukoo, au hata kujiuliza kuwa 'Daw' ina maana gani katika jina la Daw Aung San Suu Kyi? Hapa tutatazama mtindo wa pekee kabisa wa Mynmar wa kutoa majina.
Ufilipino: Mafuriko Yaathiri Vitongoji vya Jiji la Manila na Mikoa ya Karibu
Mvua kubwa ilisababisha mafuriko katika vitongoji vingi ya jiji la Manila pamoja na majimbo ya jirani katika Kisiwa cha Luzon nchini Ufilipino. Mhariri wa Global Voices aliye huko Manila, Mong Palatino, anakusanya picha kutoka katika majukwaa mbalimbali ya habari za kiraia yanayoonyesha athari kubwa ya mafuriko hayo katika mji huo mkuu wa nchi.
Tanzania, Ethiopia: Meles Zenawi ‘Atuma Twiti’ Kutoka Kilindi cha Kaburi
"@zittokabwe tafadhali uwe bora kuliko mimi nilivyokuwa. Huku juu hakuna utani, tayari ninalipia makosa yangu." Twiti iliyotumwa na Waziri Mkuu wa Ethiopia Meles Zenawi baada ya kifo chake kwenda kwa Mbunge wa Tanzania Zitto Kabwe na kuibua mjadala mtandaoni.
Syria: Mafunzo ya Silaha na Namna ya Kupigana Katika Mtandao wa Intaneti
Waasi nchini Syria wameanza kutumia YouTube ili kupeana mafunzo hasa kupitia 'Free Syrian Army Help' yaani 'Msaada wa Jeshi la Kuikomboa Syria'. Chaneli hiyo ina picha za video zipatazo 80 zikiliezea mbinu kama vile vita ya uso-kwa-uso, jinsi ya kutengeneza mabomu ya kutupwa kwa mkono, na jinsi ya kuwavizia maadui.
Morocco: Wanafunzi Wadai Marekebisho kwenye Mfumo wa Elimu
Mwezi Julai, kikundi cha wanafunzi wa nchini Morocco kilizindua ukurasa wa Facebook ulioitwa "Umoja wa Wanafunzi wa Morocco kwa ajili ya Mabadiliko ya Mfumo wa Elimu". Pungufu ya mwezi mmoja, kikundi hiki kilivuta uungwaji mkono mkubwa hasa kupitia mitandao ya kijamii.