· Juni, 2012

Below are posts about citizen media in English. Don't miss Global Voices, where Global Voices posts are translated into English! Read about our Lingua project to learn more about how Global Voices content is being translated into other languages.

Habari kuhusu Kiingereza kutoka Juni, 2012

Sudani: “Polisi Yakanusha Kutumia Risasi; Majeruhi wote ni Wakufikirika

Maafisa wa serikali ya sudani wanarudia ‘uongo’ uliozoeleka ambao watawala wa ki-Arabu wamekuwa wakitumia tangu kuanza kwa yale yanayoitwa Mapinduzi ya Uarabuni yaliyoanza mwezi Desemba 2010. Imekuwa kawaida kusikia kauli kama, ‘waandamanaji wamedhibitiwa wakati wakiwashambulia polisi, ambao nao walijihami kwa kushambulia' Watumiaji wa mtandao wanaonyesha picha tofauti wakati tetesi zinadai mtandao wa intaneti utakatwa kufuatia kuongezeka kwa maandamano.

Kenya: Kilimo cha Bustani Mijini Chashika Kasi

Nchini Kenya, wakazi wa mjijini wanajifunza mbinu mbalimbali za kulima mazao ya chakula kwa ajili ya matumizi binafzi na kwa ajili ya kuuza katika maeneo madogo. kwa watu wenye kipato kidogo au wasio na kipato, ukulima wa mijini unaweza kuwa ndiyo ufumbuzi wa kujihakikishia uwepo wa chakula. Video hizi zinaonyesha jinsi ambavyo chakula kinaweza kuzalishwa katika makasha na vifaa vingine vya kubebea kwa kutumia maeneo na rasilimali kidogo.

India: Kipindi cha Runinga cha Aamir Khan Chaweka Wazi Masuala ya Kijamii

  23 Juni 2012

Kipindi kipya cha maongezi kwenye televisheni nchi India kinachoitwa Satyamev Jayate (Ni Ukweli tu Utakaoshinda) kinachoendeshwa na muigizaji na mtengeneza filamu wa Bollywood, Aamir Khan kinaleta na kujadili miiko na masuala moto moto ya kijamii ambayo yanawanasa na kuwavutia WaHaindi wengi zaidi na zaidi. Wananchi wa kwenye mtandao wanatoa maoni yao.

Ethiopia: Ardhi, Historia na Haki katika Eneo la Gambella

Wanaharakati wa masuala ya ardhi wanatumia hati ya malalamiko ya mtandao, mtandao wa facebook na twita kufanya kampeni dhidi ya unyang’anyi wa ardhi nchini Ethiopia. Inaarifiwa kwamba wanakijiji kwenye jimbo msikini zaidi nchini humo, Gambella, wanalazimishwa kuhamia kwenye vijiji vilivyobuniwa na serikali ili kuwapisha wanaoitwa 'wawekezaji' wakubwa.

Kuhusu habari zetu za Kiingereza

en