Habari kuhusu Vita na Migogoro kutoka Januari, 2010
Colombia: Ugumu wa Kutofautisha Wazuri na Wabaya
Kwa kupitia upigaji video wa kiraia, asasi tofauti nchini Colombia zinatoa mitazamo yao kuhusu uhalifu, unyama na migogoro inayohusisha matumizi ya silaha, ambayo ni vigumu kuwatofautisha watu wazuri kutoka kwa wabaya.
Togo Yaondolewa Kwenye Mashindano ya Kombe la Afrika baada ya Shambulizi Baya
Timu ya Taifa ya Togo sasa imeondolewa rasmi kutoka kwenye mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kufuatia shambulizi lililoelekezwa kwa msafara wa timu hiyo Ijumaa iliyopita katika eneo la Kabinda lililo nchini Angola na ambalo liko kwenye ukanda wa mapigano baina ya vikosi vya serikali na vile vya waasi wanaotaka kujitenga. Huku kukiwa na shutuma nyingi kutoka kwenye serikali ya Angola na maafisa wanaosimamia soka barani Afrika, wanablogu wa Ki-Togo wanauliza maswali magumu kuhusu msiba huo.
Sudani: Je, Umoja Bado Ni Chaguo la Kimkakati
Akiandika kwa Kiarabu, mwanablogu wa Kisudani Ayman Hajj anajadili siasa za nchi yake na kwa nini watu wengi wa Sudani wanapoteza imani katika umoja.