· Januari, 2010

Habari kuhusu Uhuru wa Kujieleza kutoka Januari, 2010

Misri: wanablogu Watiwa Mbaroni Kufuatia Kutembelea kwao Naha Hammady

Leo Misri iliwatia mbaroni wanablogu 20 waliokuwa wakitembelea eneo la Naga Hammady huko Misri ya Juu ili kutoa heshima zao kwa watu waliouwawa katika shambulio la kidini mnano January 7 mwaka huu. Watu 7 waliuwawa kwa risasi huku wengine wengi wakijeruhiwa pale mwuaji alipowamiminia risasi Wakristo wa Madhehebu ya Kikopti waliokuwa wakitoka kanisani mara baada ya Misa ya Krismas (Wakopti husherehekea Krismas kila tarehe 7 Januari). Uamuzi wa kutembelea eneo hilo uliofanywa na wanablogu hao ulikuwa ni kwa lengo la kuungana dhidi ya uhasama wa kidini.

17 Januari 2010

China: Kwa Heri Google

Kufuatia tangazo la Google leo kuwa ikiwa serikali ya China haitaruhusu tawi lake la China kusitisha uzuiaji wa matokeo ya kutafuta tawi la Google nchini China litafungwa, wanamtandao walitembea mpaka...

13 Januari 2010

Thailand: “Tumechoshwa na Wizara ya Utamaduni”

Ukurasa wa wapenzi wa Facebook umezinduliwa na raia wa mtandaoni wanaokosa njia na sera za Wizara ya Utamaduni ya Thailand. Wizara hiyo imekuwa ikidhibiti sana uhamasishaji na usimamizi wa utamaduni wa asili wa Ki-Thai katika tovuti za vyombo vya habari vya kizamani na hata vile vya kisasa.

12 Januari 2010