· Aprili, 2012

Habari kuhusu Uhuru wa Kujieleza kutoka Aprili, 2012

Bangladesh: Mahakama Yaamuru Kufungwa kwa Kurasa za Facebook kwa Kukashifu Dini

Mnamo tarehe 21 Machi, mahakama moja huko Bangladesh iliziamuru mamlaka zinazohusika kuzifungia kurasa tano za Facebook na tovuti moja kwa kukashifu Mtume Mohamedi, Kuruani na dini nyinginezo. Wanaharakati wa mtandaoni wana hofu kwamba kama amri hiyo itatekelezwa, basi itafungua milango kwa uhuru wa kujieleza kudhibitiwa katika siku za usoni.

23 Aprili 2012

Ukraine: Gereza la Lukyanivska – “Mahali Watu Wanapotendewa kama Wanyama”

Mnamo tarehe 2 Aprili, Televisheni ya Ukraine ya TVi ilirusha filamu iliyotayarishwa na Kostiantyn Usov kuhusu hali ya maisha na jinsi mahabusu wanavyotendewa katika gereza la Kyiv la Lukyanivska, na pia kuhusu kuenea sana kwa rushwa miongoni mwa askari magereza. Kwa uchache, wengi katika wale ambao tayari wametazama video ya Usov walishtushwa sana na yale waliyoyaona.

6 Aprili 2012