Habari kuhusu Kiingereza kutoka Mei, 2014
Jamaika: Alama Zinapoashiria Kikomo
Blogu ya Active Voice imetoa mkusanyiko wa twiti zenye mitazamo ya kupendekeza ufumbuzi kuhusu kampeni ya #bringbackourgirls inayodai kurudishwa kwa wasichana waliotekwa na magaidi wa Boko Haram.
Baada ya Miezi Sita, Waathirika wa Kimbunga Haiyan Waendelea Kudai Msaada na Haki
Miezi sita baada ya kimbunga kikubwa kuharibu mamiliaoni ya makazi katika eneo la katikati ya Ufilipino, wahanga wanaendelea kuomba misaada na kutendelewa haki. Kuna madai ya kukosekana kwa mpango wa kurejesha hali kuwa ya kawaida.
Mashindano ya Kublogu ya AFKInsider
AFKInsider imeandaa mashindano ya kublogu ambapo mwanablogu bora kila mwezi atahitajika kuandika hadithi ya kulipiwa kila wiki kwa AFKInsider mwezi ujao: Mashindano ya wanablogu ya AFKInsider inanuia kugundua ubunifu wa wanablogu wa Biashara Afrika ambao huandika na wana nia ya teknolojia, kilimo, ujasiriamali, mali isiyohamishika, burudani, siasa, madini na habari...
Kutana na Joshua Beckford Aliyehudhuria Chuo Kikuu cha Oxford Akiwa na Umri wa Miaka 6
Blogu ya Omg Ghana iliripoti kuhusu mafanikio bora ya kielimu ya Joshua Beckford: Katika umri wa miaka 8, wewe pengine ulikuwa unafanya mazoezi ya michezo au ulikuwa ukifanya maandalizi ya kujiunga na daraja la tatu. Naam, kutana na Joshua Beckford mwenye umri wa miaka 8. Huyu yuko juu ya wastani wa...
Udikteta Umekwisha Lakini Uhuru wa Habari Bado ni Tishio Nchini Myanmar
Irrawaddy alisisitiza kuendelea kwa matatizo yanayowakabili waandishi wa habari nchini Myanmar licha ya mageuzi kutekelezwa na serikali …Licha ya mabadiliko yanayoonekana katika jinsi serikali inavyotumikia vyombo vya habari, mawazo ya msingi ni kiasi sawa kama siku za nyuma: Waandishi wamepewa “nafasi” zaidi za kufanyia kazi, lakini mipaka ya nafasi hizo...
‘Hali Mbaya’ ya Haki za Binadamu Nchini Vietnam
Mtandao wa haki za Binadamu illitoa ripoti yake ya 2013 kuhusu ‘hali mbaya’ ya haki za binadamu nchini Vietnam: …. Hali ya haki za binadamu nchini Vietnam iligeuka na kuwa mbaya mwaka 2013. Idadi ya watu waliotiwa kizuizini kwa kutoa maoni ya kisiasa yaliyo kinyume na wale wa chama tawala...
Ni kazi Ngumu Kuwa Kiongozi wa upinzani Nchini Zambia
Gershom Ndhlovu anaelezea ni kwa nini ni vigumu kuwa kiongozi wa upinzani nchini Zambia: kwa kweli ni kazi ngumu kuwa kiongozi wa upinzani nchini Zambia. Unakabiliana na polisi kila siku, hatari ya kutupiwa gesi ya machozi au hata kufungwa kwa ajili ya kufanya kazi ambayo lazima uifanye – Kukutana na...
Kwa Nini Kublogu ni Tishio kwa Serikali ya Ethiopia
Beza Tesfaye anaelezea kwa nini kublogu ni tishio kwa serikali ya Ethiopia kufuatia kukamatwa kwa wanablogu tisa Ethiopia: Ninapoandika haya, Kwa uwoga nakumbushwa kwamba nchini Ethiopia, kutoa maoni yako kunaweza kukufanya uakapewa tiketi ya daraja la kwanza gerezani. Kutoka Aprili 25 hadi 26, 2014, wanablogu tisa wa Ethiopia na waandishi...
Wakati Mgogoro wa Kisiasa Ukikolea: Thailand Kufanya Uchaguzi Mwingine Mwezi Julai
Kwa sababu ya kushindwa kwa uchaguzi wa mwezi Februari kutatua mgogoro wa kisiasa nchini Thailand, uchaguzi mwingine umepangwa kufanyika Julai 20. Lakini je, upinzani utasusia kwa mara nyingine?
China Yamweka Kizuizini Mwanasheria wa Haki za Binadamu Pu Zhiqiang
Hii si mara ya kwanza kwa Pu Zhiqiang kuwekwa kizuizini. Akiwa mkosoaji maarufu wa sera za serikali ya China, amekuwa akifuatiliwa kwa karibu na vyombo vya usalama wa nchi hiyo.