Kutana na Joshua Beckford Aliyehudhuria Chuo Kikuu cha Oxford Akiwa na Umri wa Miaka 6

Blogu ya Omg Ghana iliripoti kuhusu mafanikio bora ya kielimu ya Joshua Beckford:

Katika umri wa miaka 8, wewe pengine ulikuwa unafanya mazoezi ya michezo au ulikuwa ukifanya maandalizi ya kujiunga na daraja la tatu. Naam, kutana na Joshua Beckford mwenye umri wa miaka 8. Huyu yuko juu ya wastani wa mtu mwenye umri wa miaka 8. Alisoma katika Chuo Kikuu cha Oxford akiwa na umri wa miaka 6, na ni mfano wa kampeni ya wagonjwa wa akili katika jamii ya watu weusi na wachache (BME). Kampeni hiyo ilianzishwa ili kuonyesha vikwazo watu wenye asili ya weusi ambao mara nyingi hukutana nayo wanapojaribu kupata huduma ya kusaidia na huduma wanazohitaji. Beckford ni wa pekee, yuko juu zaidi kwa Kiwango cha daraja la shule alilohitajika na ilimlazimu kusomea nyumbani. Yeye hufanya vizuri katika Hesabu, Lugha za Kigeni, historia, falsafa, teknolojia na Sayansi.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.