Habari kuhusu Kiingereza kutoka Disemba, 2009
Misitu ya Madagascar Inateketezwa kwa $460,000 kwa Siku
Wakati mataifa ya dunia yanakutana huko Copenhagen kwa ajili ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi, Madagascar, ambayo imekwishapoteza 90% ya misitu yake ya asili, inakabiliwa na tishio la biashara ya magendo ya magogo, inayotishia kuharibu kile kilichobakia katika moja ya mifumo ya mazingira yenye viumbe na mimea mingi inayotofautiana.
Ethiopia: Meles Zenawi aisaliti Afrika
Lucas Liganga aandika kuhusu usaliti wa Waziri Mkuu wa Ethiopia: “kwa bahati mbaya, Waziri Mkuu wa Ethiopia meles Zenawi ambaye ni msemaji wa Afrika kuhusu mabadiliko ya tabianchi amejiunga na Ufaransa na kubadili nakala ya Afrika, jambo ambalo limewastua wajumbe wa Afrika.”
Morocco: Mwanablogu Mwingine Atupwa Gerezani
Mnamo tarehe 14 Desemba, siku ya Jumatatu, mwanablogu Bashir Hazzam na mmiliki wa mgahawa wa Intaneti Abdullah Boukhou walihukumiwa kifungo cha miezi minne jela kwa huyo wa kwanza na mwaka mmoja kwa huyo wa pili pamoja na kulipa faini ya MAD 500 (sawa na dola za Marekani 63) kila mmoja katika mahakama ya Goulmim.
Misri: Makao Makuu ya Kuzimu Duniani
Wanablogu na wanaharakati wengi wa Kimisri wamekuwa wakikamatwa na Usalama wa Taifa katika nyakati tafauti kwa sababu mbalimbali –za kweli au za bandia –Wa7da Masreya aliwahoji wanablogu mbalimbali na kuweka makala ya kina kuhusu mbinu za utesaji na hila za kisaikolojia ambazo wanablogu wale wamekuwa wakikumbana nazo kwenye makao makuu ya Usalama wa Taifa katika wilaya ya Jiji la Nasr.
China: Kujitoa Uhai kwa Msomi Mwingine tena – Kisa cha Yang Yuanyuan
YANG Yuanyuan, binti msomi mwenye miaka 30 aliyekuwa na shahada ya uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Shanghai Maritime, alijinyonga kwenye bafu la nyumbani kwake mnamo Novemba 25 mwaka huu. Siku moja kabla hajachukua uamuzi huo alimwambia mama yake kwamba maarifa hayawezi kubadili majaaliwa. Miaka ya hivi karibuni imeshuhudia ongezeko la...
Canada Imesema Nini? Upotoshaji wa Habari Kwenye Mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi
Serikali ya Canada inasemekana imetoa tamko la jazba leo, ikikanusha upotoshaji wa habari zinazodaiwa kufanywa nayo kwa mujibu wa Jarida la Wall Street likidai kwamba Canada imebadili sera yake na itakuwa ikikubaliana na malengo ya kupunguza hewa ya ukaa.
Wapiga picha wa Kiafrika, waandishi na wasanii wapata sauti zao kwenye blogu
Kadri Waafrika wengi wanavyozidi kugundua nguvu ya kublogu kama zana ya kutoa maoni kwa kiwango cha dunia nzima, tarakimu ya wanablogu imeongezeka na pia maudhui yanayopewa kipaumbele. Kwa tarakimu hiyo ya kukua kwa blogu, wasanii wengi wa Kiafrika wamejiunga, na ongezeko kubwa likionekana kwenye blogu za mashairi kama ilivyo kwa upigaji picha unaochipukia na blogu za sanaa za maonyesho. Tunazipitia baadhi.
Israel: Kublogu Kwa Ajili Ya Mazingira Nchini Jordan
“Wanamazingira na Waandishi kutoka Palestina, Jordan na Israel watakutana huko Madaba, Jordan mwezi huu kwa ajili ya warsha ya siku 2: “Kublogu kwa Ajili ya Mazingira” tarehe 20-21 Desemba,” anaandika Muisrael Green Prophet, kwenye Mideast Youth.
Barbados, Trinidad & Tobago:Plastiki na Uchafuzi wa Mazingira
“Fanya matembezi kwenye pwani yoyote nchini Barbados – na utaona uchafu wa plastiki uliosukumwa ufukweni”: Barbados Free Press anauliza kama uuzaji wa chupa za plastiki za maji uwekewe vikwazo, wakati Mtrinidadi Keith Francis pia anaguswa na suala la uchafuzi wa mazingira kwa plastiki ulimwenguni.
Tunisia: Mwanafunzi Atupwa Gerezani kwa Kuhojiwa na Chombo cha Habari
Wanaharakati nchini Tunisia wamezindua ukurasa wa Facebook na blogu ili kumuunga mkono Mohamed Soudani, 24, aliyetoweka mnamo tarehe 22 Oktoba 2009 nchini humo mara baada ya kufanya mahojiano na Redio Monte Carlo International na vilevile Redio France International. Tangia hapo marafiki walipata fununu kwamba alikamatwa na kutupwa korokoroni na kuteswa vibaya.