makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mosi Simba
Saudi Arabia: Mfalme Awaahidi Wananchi wa Saudia Fedha Zaidi
Fedha zaidi zimeahidiwa kutolewa kwa wananchi wa Saudia, ahadi ambayo Mfalme Abdulla ameitoa kupitia hotuba yake kwa taifa leo. Katika hotuba hiyo iliyokuwa fupi, Mlinzi wa Misikiti Miwili Mitukufu aliwashukuru viongozi wa dini, waandishi na Wizara ya Mambo ya Ndani kwa juhudi walizofanya kutetea ufalme. Matamko na Amri vilifuata ya kwamba mabilioni yatagawanywa kwa watu wa Saudia.
Tanzania: Majumuisho ya Habari za Uchaguzi Mkuu wa 2010
Mnamo tarehe 31 Oktoba 2010, Watanzania watashiriki katika uchaguzi wa Rais wa Muungano, Rais wa Zanzibar pamoja na Wabunge na Wawakilishi katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar. Huu ni mjumuisho wa yale yaliyojiri katika blogu mbalimbali kuhusiana na uchaguzi huo.
Tanzania: Ulimwengu wa Blogu Wachambua Kampeni za Uchaguzi Mkuu 2010
Ifikapo tarehe 31 Oktoba 2010, Watanzania zaidi ya milioni 19.6 watafanya uamuzi muhimu kuhusu hatma ya nchi yao. Watafanya hivyo kupitia uchaguzi mkuu wa nne chini ya mfumo wa vyama vingi. Wakati zimebaki siku chache kabla ya uchaguzi huo, ulimwengu wa blogu wa Tanzania nao unafuatilia kwa karibu yale yanayotokea katika kampeni za vyama mbalimbali.
Moroko: Kupinga Mateso Sehemu Moja; Kupinga Mateso Kila Sehemu
Wanablogu wa Moroko wamekuwa wakionyesha kukasirishwa kwao juu ya tabia ya kutojali ya vyombo vya habari vikubwa na unafiki wa serikali yao kufuatia kifo cha kijana wa KiMoroko mikononi mwa wawakilishi wa serikali.
Urusi: Wanablogu wakutana na Balozi wa Irani, waepa kuhoji masuala nyeti
Mkutano kati ya wanablogu wanaoongoza nchini Urusi na Balozi wa Irani jijini Moscow, siku tatu tu baada ya mwanablogu Hossein Derakshan kuhukumiwa kifungo cha miaka 19.5 jela kwa kile kilichoelezwa kuwa ni "kufanya propaganda zinazoipinga serikali" ulizionyesha wazi juhudi zisizoeleweka za diplomasia ya mtandaoni ya Irani nchini Urusi. Vilevile ulionyesha jinsi maslahi binafsi ya kibiashara pamoja na mtizamo taharuki uliopita kiasi wa baadhi ya wanablogu maarufu wa Urusi.
Tanzania: Matumizi ya Vyombo vya Habari vya Kijamii kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2010 Nchini Tanzania
Tanzania inaelekea katika uchaguzi wake mkuu mnamo Oktoba 31 mwaka huu na hivi sasa kampeni za uchaguzi zinaelekea kileleni. Wakati kampeni zikipamba moto, wagombea wa nafasi ya urais, ubunge na udiwani wameanza kutumia zana mpya za mawasiliano ya jamii ili kuwasiliana na wapiga kura. Sanjari na mikutano ya kampeni, ambayo hulenga watu wengi zaidi, idadi ndogo ya wanasiasa wameanza kutumia zana za mawasiliano ya kijamii kama vile blogu, picha za video za mtandaoni, Facebook na Twitter ili kukuza mawasiliano na wapiga kura.
Irani: Huenda Mwanablogu Aliyefungwa, Hossein Derakhshan (”Hoder”), Akakabiliwa na Hukumu ya Kifo
Mwendesha mashtaka huko Tehrani anataka mwanablogu wa Irani aliye gerezani Hossein Derakhshan ("Hoder") apewe adhabu ya kifo. Hakimu bado hajatoa uamuzi. Derakhshan anashtakiwa kwa kosa la “kushirikiana na dola adui, kutangeneza propaganda dhidi ya utawala wa Kiislamu, kutusi utukufu wa dini, na kutengeneza propaganda kwa ajili ya matumizi ya vikundi vinavyopinga mapinduzi." Alitiwa nguvuni miezi 22 iliyopita.
Bahraini: Ali Abdulemam, mwanablogu na mchangiaji wa Global Voices akamatwa
Ali Abdulemam, mwanablogu maarufu wa nchini Bahraini na mwandishi wa Kitengo cha Utetezi cha Global Voices, amekamatwa mapema leo na mamlaka ya nchi ya Bahraini kwa kile anachotuhumiwa nacho kwamba anasambaza “habari za uongo” kupitia mtandao wa BahrainOnline.org, ambao ni moja ya mitandao maarufu zaidi nchini humo inayopigania kuwepo kwa...
Msumbiji: Maputo katika Hali ya Tahadhari Kutokana na Machafuko
Jiji la Maputo lipo kwenye hali ya tahadhari wakati machafuko yakisambaa kutokana na kupanda kwa bei ya mkate, maji na umeme. Wakazi wanataarifu kuwepo kwa vurugu mitaani huku hali ikizidi kuwa mbaya.
Tunisia: Picha ‘Zilizochakachuliwa’ ni Dalili ya Hali Halisi katika Vyombo vya Habari vya Kitaifa
Utumiaji vyombo vya habari vya kitaifa nchini Tunisia kama chombo vya kupigia propaganda ni jambo ambalo limeripotiwa vya kutosha. Ushahidi wa hivi karibuni kabisa wa utumiaji mbaya wa vyombo vya habari umewekwa bayana na wanablogu wa nchi hiyo mnamo tarehe 20 Agosti baada ya magazeti ya Le Temps na Assabah kuchapisha ripoti kuhusu taasisi ya hisani ya Zeitouna kutuma msaada wa kibinadamu wa chakula kwa waathirika wa mafuriko nchini Pakistani.