makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mosi Simba kutoka Machi, 2010
Serikali ya Japani: Kuhusu Kuanguka kwa Mfumo wa Ajira
Chombo kinachotumika kufanya tafakari nzito cha Baraza la Mawaziri la Japani, Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (内閣府 経済社会総合研究所)(ESRI) kimechapisha matokeo ya utafiti yaliyopima hadhi ya sasa ya ajira...
Jamhuri ya Dominika: Upinzani Dhidi ya Shughuli za Kampuni ya Uchimbaji Dhahabu ya Barrick
Kumekuwa na ongezeko la upinzani dhidi ya shughuli za Kampuni ya Uchimbaji Dhahabu ya Barrick kwenye Jamhuri ya Dominika kwa sababu ya vipengele vilivyo kwenye mkataba na manufaa ya dola hilo, vilevile kutokana na sababu mbalimbali za kimazingira.
Siku ya Ada Lovelace: Kuwapongeza Wanawake Wanajishughulisha Kupigania Teknolojia na Uwazi Ulimwenguni
Katika kusherehekea Siku ya Ada Lovelace tunawaletea makala fupifupi kuhusu wanawake kadhaa walio sehemu mbalimbali duniani ambao hutumia teknolojia ili kuzifanya serikali ziwe wazi na zinazowajibika zaidi.
Global Pulse 2010: Mwaliko wa kuzungumza na watoa uamuzi mtandaoni
Kuanzia tarehe 29 hadi 31 Machi, vuguvugu linalojulikana kama Global Pulse 2010, yaani Mapigo ya Moyo ya Ulimwengu 2010, linakusudia kuwakusanya jumla ya watu 20,000 kupitia mtandao ili wafanya mazungumzo kuhusu mada mbalimbali kuanzia zinazohusu maendeleo ya binadamu hadi sayansi na teknolojia.
China: Uchi Ulio Rasmi
Serikali moja ya mji huko katika Jimbo la Sichuan sasa inaitwa “Serikali ya Kwanza nchini China Iliyo Uchi kabisa” baada ya kuwa maafisa wa mji huo kuweka mishahara na matumizi...
Pakistani: Vitendo vya Unyanyasaji Watoto Vyaongezeka
Msemo 'Unyanyasaji watoto' hutumika kueleza vitendo vya aina mbalimbali vilivyo jinai na vinavyofanywa dhidi ya watoto. Wanablogu wanajadili vitendo hivi vya unyanyasiaji watoto vinavyokera na vinavyozidi kuongezeka nchini Pakistani.
Misri: Wafanyakazi wa IslamOnline Wagoma
Mamia ya wafanyakazi, wahariri, na waandishi wa habari walianza mgomo wa kuonyesha hasira yao katika mtandao unaosomwa sana wa jiji la Cairo unaojulikana kwa jina la Islamonline baada ya kuwa wafanyakazi wapatao 250 wamefukuzwa kazi. Kwa mara ya kwanza, wagomaji wanatumia kwa ufanisi na vizuri kabisa aina mpya ya chombo cha habari ili kuvuta usikivu na uungwaji mkono katika kile wanachokipigania, kuanzia na Twita inayoendelea mpaka mmiminiko wa habari wa hapo kwa hapo.
Mwaka Mmoja Baada ya Mapinduzi, Viongozi wa Madagaska Wakabiliwa na Vikwazo
Machi 17, 2009 nchini Madagaska, vikwazo vinavyowalenga viongozi wa sasa wa Madagaska vinaandaliwa kwa kushindwa kwao kuheshima makubaliano ya Maputo ambayo hapo awali yalifikiwa na pande zote zinazohusika. Matokeo ya vikwazo hivyo ni pamoja na kuzuiwa kwa mali zinazozalisha fedha na pengine kukamatwa kwa wanaohusika endapo watasafiri nje ya nchi.