Mosi Simba · Disemba, 2009

makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mosi Simba kutoka Disemba, 2009

Morocco: Mwanablogu Mwingine Atupwa Gerezani

Mnamo tarehe 14 Desemba, siku ya Jumatatu, mwanablogu Bashir Hazzam na mmiliki wa mgahawa wa Intaneti Abdullah Boukhou walihukumiwa kifungo cha miezi minne jela kwa huyo wa kwanza na mwaka mmoja kwa huyo wa pili pamoja na kulipa faini ya MAD 500 (sawa na dola za Marekani 63) kila mmoja katika mahakama ya Goulmim.

20 Disemba 2009

Tunisia: Mwanafunzi Atupwa Gerezani kwa Kuhojiwa na Chombo cha Habari

Wanaharakati nchini Tunisia wamezindua ukurasa wa Facebook na blogu ili kumuunga mkono Mohamed Soudani, 24, aliyetoweka mnamo tarehe 22 Oktoba 2009 nchini humo mara baada ya kufanya mahojiano na Redio Monte Carlo International na vilevile Redio France International. Tangia hapo marafiki walipata fununu kwamba alikamatwa na kutupwa korokoroni na kuteswa vibaya.

15 Disemba 2009

Brazil: Wito wa Kugomea Gazeti Linaloongoza Nchini

Wanablogu wa Brazili wamekuwa wakihamasisha mgomo dhidi ya kile walichokiita Coupist Press Party, yaani Sherehe ya Chombo cha Habari ya Kutaka Kupindua Serikali, kwa hiyo wamekuwa wakiwataka watu kuacha kununua, kusoma au kutoa maoni na badala yake kufuta usajili wao kutoka kwenye gazeti la Folha de São Paulo na tovuti yake.

14 Disemba 2009

Indonesia: Sarafu za Kudai Haki

Raia wa mtandaoni (Netizens) wamezindua kampeni ya kukusanya fedha zilizo katika muundo wa sarafu ili kumuunga mkono Prita Mulyasari, mama wa nyumbani raia wa Indonesia aliyeandika malalamiko yake mtandaoni dhidi ya hospitali iliyotoa huduma mbaya, na ambaye alipatikana na hatia na mahakama moja ya kosa la "kuchafua jina" la hospitali hiyo binafsi.

8 Disemba 2009

Guatemala: Kuvunja Milango ya Madanguro

Blogu inayojulikana kama Noticias para Dios inatoa habari za ndani, kama vile mambo yenyewe yanavyotokea pasipo kuficha kitu, kuhusu maisha ya kila siku ya mwanasheria wa Ki-Guatemala anayejaribu kuwaokoa watoto kutoka kwenye madanguro ambako wamekuwa wakiishi baada ya kuchukuliwa kutoka makwao.

6 Disemba 2009