Mosi Simba · Aprili, 2011

makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mosi Simba kutoka Aprili, 2011

Misri: Mubarak awekwa Kizuizini

Miezi michache tu iliyopita, raia wengi wa Misri walitamani sana kumwona aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Rais Mubarak, akitupwa jela, hata hivyo, pengine ni wachache miongoni mwao waliofikiri kwa uhakika kabisa kwamba siku moja jambo hili lingetimia. Hata hivyo, mnamo Jumatano ya tarehe 13 Aprili, 2011, raia wa Misri waliamka na mapema asubuhi ya siku hiyohiyo kukutana na habari zinazohusu Mubaraka kutupwa kizuizini. Hapa chini tunawaletea jinsi habari hizi zilivyopokelewa katika ulimwengu wa uandishi wa habari wa Kijmii miongoni mwa Wamisri.

22 Aprili 2011

Myanmar: Simulizi za Wafanyakazi wa Misaada Baada ya Tetemeko la Ardhi

Myanmar bado inasumbuka kutokana na tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 6.8 ambalo liliikumba nchi hiyo. Mwandishi wetu aliyeko Myanmar anatafsiri mahojiano na simulizi za wakazi pamoja na wafanyakazi wa misaada ambao walishuhudia kiwango cha uharibifu uliofanywa na tetemeko hilo kaskazini mashariki mwa Myanmar.

10 Aprili 2011

Bahrain: Waandishi wa Habari Wazuiwa Kuingia Wakiwa Uwanja wa Ndege

Bahrain iliingia kwenye vurugu kubwa zilizoambatana na polisi kutumia nguvu dhidi ya waandamanaji waliopiga kambi katika eneo muhimu la wazi linalohusudiwa sana liitwalo Lulu Jumatano iliyopita. Mchana wa siku hiyo nilipanda ndege inayotoka Doha, nchini Qatar, kwenda Bahrain, kwa upande mmoja nikitaka kujionea mwenyewe nini kilikuwa kikitokea katika nchi hii ya kisiwa ambayo ilipata kuwa nyumbani kwangu. Saa kadhaa baadaye nilijikuta kwenye ndege ya kurudi Doha, baada ya kunyimwa ruhusa ya kupita pale uwanja wa ndege.

9 Aprili 2011

Wanablogu wa Kenya Waunda Umoja; BAKE

Mnamo tarehe 25 Machi, wanablogu kadhaa wa Kenya walifanya mkutano katika mji mkuu wa nchi hiyo, Nairobi, mkutano uliitishwa na BAKE (Bloggers Association KEnya). Huo ulikuwa mkutano wa 4 uliotokana na msukumo wa wanablogu wakongwe wa Kenya.

4 Aprili 2011

Saudi Arabia: Mfalme Awaahidi Wananchi wa Saudia Fedha Zaidi

Fedha zaidi zimeahidiwa kutolewa kwa wananchi wa Saudia, ahadi ambayo Mfalme Abdulla ameitoa kupitia hotuba yake kwa taifa leo. Katika hotuba hiyo iliyokuwa fupi, Mlinzi wa Misikiti Miwili Mitukufu aliwashukuru viongozi wa dini, waandishi na Wizara ya Mambo ya Ndani kwa juhudi walizofanya kutetea ufalme. Matamko na Amri vilifuata ya kwamba mabilioni yatagawanywa kwa watu wa Saudia.

3 Aprili 2011