Mosi Simba · Aprili, 2010

Ni mpenzi wa lugha ya Kiswahili. Licha ya kuwa ni mhariri na mwandishi wa vitabu, mimi pia ni mfasiri. Nafasiri maandiko kutoka lugha ya Kiingereza kuja Kiswahili na kutoka Kiswahili kwenda Kiingereza. Pia ni mwanablogu: http://simbadeo.wordpress.com Ndiyo kusema kuwa ninapenda kuperuzi kwenye kurasa za mtandaoni ili kuilisha akili kwa habari mbalimbali zinazojiri huku na huko duniani. Ni raia wa Tanzania na mkaazi wa Dar es Salaam. Karibu.

Anwani ya Barua Pepe Mosi Simba

makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mosi Simba kutoka Aprili, 2010

Kirigistani: Mapinduzi “Yaliyowekwa kwenye Kumbukumbu”

RuNet Echo  11 Aprili 2010

Mnamo tarehe 6 April, nchi ya Kirigistani ilikumbwa na maandamano makubwa ya kupinga utawala ambayo hatimaye yaliing'oa serikali pamoja na kusababisha vifo vya watu wengi. Pamoja na kwamba intaneti haikushika usukani katika kuhamasisha maandamano hayo, imetumika sana katika kuhifadhi kumbukumbu za kina za maandamano hayo.

Moroko: Je, Wakristu Wako Hatarini?

Mapema mwezi Machi mwaka huu, watazamaji walishuhudia jumla ya wafanyakazi wa muda mrefu katika kituo cha Kikristo cha kulelea watoto yatima wapatao 20 wakifukuzwa kutoka katika nchi ambayo wanaiona kama nyumbani. Tukio hilo pamoja na mengine kadhaa yaliyofuatia yamezusha mjadala kuhusiana na imani ya Kikristu katika ufalme huo.