Ni mpenzi wa lugha ya Kiswahili. Licha ya kuwa ni mhariri na mwandishi wa vitabu, mimi pia ni mfasiri. Nafasiri maandiko kutoka lugha ya Kiingereza kuja Kiswahili na kutoka Kiswahili kwenda Kiingereza. Pia ni mwanablogu: http://simbadeo.wordpress.com Ndiyo kusema kuwa ninapenda kuperuzi kwenye kurasa za mtandaoni ili kuilisha akili kwa habari mbalimbali zinazojiri huku na huko duniani. Ni raia wa Tanzania na mkaazi wa Dar es Salaam. Karibu.
makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mosi Simba kutoka Aprili, 2010
Kirigistani: Mapinduzi “Yaliyowekwa kwenye Kumbukumbu”
Mnamo tarehe 6 April, nchi ya Kirigistani ilikumbwa na maandamano makubwa ya kupinga utawala ambayo hatimaye yaliing'oa serikali pamoja na kusababisha vifo vya watu wengi. Pamoja na kwamba intaneti haikushika usukani katika kuhamasisha maandamano hayo, imetumika sana katika kuhifadhi kumbukumbu za kina za maandamano hayo.
Brazili: Ulimwengu wa blogu waunga mkono sheria ya kuzuia ufisadi
Muswada wa sheria kwa ajili ya kuwazuia wanasiasa ambao wamewahi kutenda makosa makubwa ya jinai ili wasigombee nafasi za kuchaguliwa umeanza kuzua kizaazaa nchini Brazili huku karibu watu milioni 2 wakitia saini zao kama ishara ya kuunga mkono.
Moroko: Je, Wakristu Wako Hatarini?
Mapema mwezi Machi mwaka huu, watazamaji walishuhudia jumla ya wafanyakazi wa muda mrefu katika kituo cha Kikristo cha kulelea watoto yatima wapatao 20 wakifukuzwa kutoka katika nchi ambayo wanaiona kama nyumbani. Tukio hilo pamoja na mengine kadhaa yaliyofuatia yamezusha mjadala kuhusiana na imani ya Kikristu katika ufalme huo.
Chile: Mchakato wa Ujenzi Mpya Baada ya Tetemeko la Ardhi
Mwezi mmoja baada ya tetemeko baya kabisa nchini Chile, Rais Sebastián Piñera ametangaza mpango wa ujenzi mpya wa miundombingu ya nchi na majengo, akiwataka raia wa Chile kutoa mapendekezo jinsi gani mchakato huo utekelezwe na kusimamiwa.