Mosi Simba · Machi, 2012

Ni mpenzi wa lugha ya Kiswahili. Licha ya kuwa ni mhariri na mwandishi wa vitabu, mimi pia ni mfasiri. Nafasiri maandiko kutoka lugha ya Kiingereza kuja Kiswahili na kutoka Kiswahili kwenda Kiingereza. Pia ni mwanablogu: http://simbadeo.wordpress.com Ndiyo kusema kuwa ninapenda kuperuzi kwenye kurasa za mtandaoni ili kuilisha akili kwa habari mbalimbali zinazojiri huku na huko duniani. Ni raia wa Tanzania na mkaazi wa Dar es Salaam. Karibu.

Anwani ya Barua Pepe Mosi Simba

makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mosi Simba kutoka Machi, 2012

India: Gazeti pekee duniani linaloandikwa kwa mkono

  31 Machi 2012

Magazeti ya mwanzo yalikuwa yakiandikwa kwa mkono. Inawezekana kwamba hivi sasa gazeti la ‘The Musalman‘ pengine ndiyo pekee lililobaki linaloandikwa kwa mkono ulimwenguni. Gazeti hili linalochapishwa kwa lugha ya Ki-Urdu lilianzishwa mwaka 1927 na Chenab Syed Asmadullah Sahi ambapo hivi sasa linachapishwa kila siku katika jiji la Chennai huko India tangu kuanzishwa kwake.The earliest forms of newspaper were handwritten and now 'The Musalman' probably is the last handwritten newspaper in the world. This Urdu language newspaper was established in 1927 and has been published daily in the Chennai city of India ever since.