Ni mpenzi wa lugha ya Kiswahili. Licha ya kuwa ni mhariri na mwandishi wa vitabu, mimi pia ni mfasiri. Nafasiri maandiko kutoka lugha ya Kiingereza kuja Kiswahili na kutoka Kiswahili kwenda Kiingereza. Pia ni mwanablogu: http://simbadeo.wordpress.com Ndiyo kusema kuwa ninapenda kuperuzi kwenye kurasa za mtandaoni ili kuilisha akili kwa habari mbalimbali zinazojiri huku na huko duniani. Ni raia wa Tanzania na mkaazi wa Dar es Salaam. Karibu.
makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mosi Simba kutoka Septemba, 2010
Irani: Huenda Mwanablogu Aliyefungwa, Hossein Derakhshan (”Hoder”), Akakabiliwa na Hukumu ya Kifo
Mwendesha mashtaka huko Tehrani anataka mwanablogu wa Irani aliye gerezani Hossein Derakhshan ("Hoder") apewe adhabu ya kifo. Hakimu bado hajatoa uamuzi. Derakhshan anashtakiwa kwa kosa la “kushirikiana na dola adui, kutangeneza propaganda dhidi ya utawala wa Kiislamu, kutusi utukufu wa dini, na kutengeneza propaganda kwa ajili ya matumizi ya vikundi vinavyopinga mapinduzi." Alitiwa nguvuni miezi 22 iliyopita.
Bahraini: Ali Abdulemam, mwanablogu na mchangiaji wa Global Voices akamatwa
Ali Abdulemam, mwanablogu maarufu wa nchini Bahraini na mwandishi wa Kitengo cha Utetezi cha Global Voices, amekamatwa mapema leo na mamlaka ya nchi ya Bahraini kwa kile anachotuhumiwa nacho kwamba anasambaza “habari za uongo” kupitia mtandao wa BahrainOnline.org, ambao ni moja ya mitandao maarufu zaidi nchini humo inayopigania kuwepo kwa...
Msumbiji: Maputo katika Hali ya Tahadhari Kutokana na Machafuko
Jiji la Maputo lipo kwenye hali ya tahadhari wakati machafuko yakisambaa kutokana na kupanda kwa bei ya mkate, maji na umeme. Wakazi wanataarifu kuwepo kwa vurugu mitaani huku hali ikizidi kuwa mbaya.