Habari kuhusu Kiingereza kutoka Disemba, 2013
Sababu za Ajali Barabarani Mjini Bangkok
Cha kushangaza, polisi mjini Bangkok, Thailand wanadai kwamba asilimia 30 ya ajali za barabarani husababishwa na ‘magari yasiyostahili kuwa barabarani’ wakati yanayo endeshwa kasi ni asilimia 5 ya ajali. Mwandishi Thitipol Panyalimpanun anabainisha kuwa katika nchi nyingi, ajali za barabarani hulaumiwa kwa makosa dereva na si juu ya magari.
Caribbean: Kwaheri, Nelson Mandela
Tangazo la kifo cha Nelson Mandela limepokelewa kwa mshtuko. Wanablogu wa maeneo mbalimbali wanashirikishana mawazo yao kuhusu kuondoka kwa mmoja wa magwiji wa upinzani kwa njia za amani duniani aliyetutoka.
#Mambo52KuhusuTanzania katika Kusherekea Miaka 52 ya Uhuru
Tanzania Bara ilisherehekea miaka 52 ya uhuru wake tarehe 9 Desemba, 2013. Katika kusherehekea siku hiyo, alama habari ya #Mambo52KuhusuTanzania ilitumika kushirikishana takwimu na mambo halisi kuhusu nchi hiyo.
Wanafunzi 3,000 Wafanya Maandamano dhidi ya Mageuzi ya Elimu Nchini Gabon
Mageuzi ya mfumo wa elimu yaliahirishwa [fr] nchini Gabon baada ya walimu na wanafunzi kuandamana pamoja kwa maandamano. Katika mapendekezo ya mageuzi, mitihani ya mwisho ili kupata diploma ya shule ya sekondari itafanyika katika duru moja badala ya mbili na kuingia katika shule ya sekondari zitafanyiwa mtihani wa mwisho badala...
Urusi: Kupigwa Risasi Mgeni na Hisia za Wazi za Ubaguzi wa Rangi
Kitendo cha kijana mmoja kupigwa risasi Novemba 23, 2013 kwenye treni ya Moscow kimeibua mjadala mpya mtandaoni kuhusu harakati zenye msimamo mkali Urusi kubagua wahamiaji nchini humo.
Wanaijeria Wamkumbuka Nelson Mandela
Nelson Mandela, mzalendo mpendwa na mshindi wa tuzo ya Amani ya Nobel, amefariki Desemba 5, 2013. Wanaijeria wanakumbuka kumbumbuku iliyoachwa nyuma na Rais huyo wa kwanza wa Afrika Kusini
Hekima 17 za Nelson Mandela Zinazofaa Kusomwa na Kila Mmoja
Nelson Mandela, Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, anaendelea kuzungumza na ulimwengu kupitia watumiaji wa mtandao wa twita waliopokea taarifa za kifo chake kwa kusambaza nukuu za maneno yake ya kukubukwa.
Misri: Kampeni kwa Ajili ya Haki za Watu Wenye Mahitaji Maalum
Wamisri pembezoni wenye mahitaji maalum wamekuwa wakifanya maandamano kwa haki zao kabla na tangu mapinduzi ya #Jan25. Hata hivyo, malalamiko yao bado hayajatatuliwa. Wakati Kamati ya watu 50 wanapiga kura juu ya rasimu ya hivi karibuni zaidi ya Katiba ya Misri, kampeni ya Zayee Zayak, ambayo hutafsiriwa kuwa “Mimi ni...
Mkutano: Kutengeneza Dunia Halisi ya Sauti za Dunia kwa Hadhira Halisi
Katika toleo hili la GV Face tunakutana na jopo la magwiji wa wawezeshaji wa mikutano ya Global Voices kutoka Misri, Pakistan, na Ureno.
Taiwan: Maandamano Dhidi ya Sheria Juu ya Usawa Kwenye Ndoa
Wabunge wa Yuan nchini Taiwan walipitisha muswada wa kwanza ya “Usawa kwenye Ndoa“ [zh] mnamo Oktoba 25, 2013. Novemba 30, zaidi ya watu 300,000 walipinga muswada huu, hasa dhidi ya pendekezo juu ya ndoa za jinsia moja. J. Michael Cole, mwandishi wa habari wa kujitegemea mkaazi wa Taipei, alielezea kile...