makala mpya zaidi zilizoandikwa na j nambiza tungaraza kutoka Januari, 2010
Picha ya Dunia Katika Siku ya Kupinga Rushwa Duniani
Katika matayarisho ya uzinduzi wa mtandao wa teknolojia na Uwazi, hii ni makala ya kwanza kabisa katika mfululizo wa makala ambazo zitavinjari mada zinazohusiana kwa kupitia macho ya wanablogu wa dunia.
Georgia: Hebu Tuongelee Tendo la Ngono…
Pengine mada iliyotawala katika vyombo vya uanahabari wa kijamii vya Georgia haikuwa siasa, uchaguzi, matatizo, matetemeko ya ardhi au majanga. Badala yake, mada iliyojadiliwa sana ilikuwa inahusu kipindi kipya cha televisheni, Ghame Shorenastan. Kinachoonyeshwa kwenye Imedi TV, jina la kipindi hicho linatafsirika kama Usiku pamoja na Shorena na kinaongelea mada zinazohusu tendo la ngono.
Msumbiji: Kifo Cha Mradi Mkubwa wa Mazao Nishati
Mwishoni mwa mwezi Disemba, Baraza la Mawaziri la Msumbiji lilitoa tamko muhimu. Kibali cha kutumia Hekta 30,000 za ardhi kwa kampuni ya mazao nishati (biofuels) Procana, kimebatilishwa. Shauri la Mradi wa Procana, ulipo kwenye eneo kubwa linalopakana na Mbuga ya Taifa ya Limpopo ambayo imetanda mpaka nje mpaka wa nchi, lilikuwa na utata pamoja na mvutano mkubwa tangu (shauri hilo) lilipoanza mwanzoni mwa mwaka 2007.
Australia: Mauaji ya Mhindi Yazua Mzozo
Mauaji ya mtu mwenye asili ya India mjini Melbourne yamewasha tena mjadala kuhusu ubaguzi wa rangi nchini Australia na usalama wa wanafunzi kutoka ng’ambo. Kadhalika yameathiri uhusiano kati ya Australia na India. Mwandishi wa GV Kevin Rennie anakusanya maoni ya wanablogu wa Australia.
Sri Lanka: Kulipia Vyombo Vya Kimataifa Vya Habari kwa Ajili ya Uchaguzi wa Ndani
Kampeni kabambe ya Rais wa Sri Lanka aliye madarakani, Mahinda Rajapakshe inajumuisha manunuzi ya nafasi za matangazo katika tovuti mashuhuri za vyombo vya habari duniani. Groundviews anahoji sababu ya kuvilipa vyombo vya habari vya kimataifa kwa ajili ya uchaguzi wa ndani ya nchi.
Lebanoni: Matukio ya Wafanyakazi Kujiua ‘Yanadharauliwa’
Matthew Cassel anaripoti tukio la kujia la Theresa Seda, mfanyakazi wa ndani wa Kifilipino jijini Beirut. Soma habari za kina za kutisha za jinsi vifo vya namna hiyo vinavyoongezeka kwa idadi – vinaendelea kutotiliwa maanani kwenye Justimage.
Kenya: Video ya Fundi Baiskeli na Vifaa vya Kienyeji
Katika blogu ya Afrigadget kuna video ya fundi baiskeli anayeonyesha na kuelezea jinsi ya kutumia zana alizozitengeneza nyumbani wakati anafanya kazi zake katika soko jijini Nairobi.
China na Hong Kong: Walinzi na Wauaji
Bodyguards and Assassins (Walinzi na Wauaji) ni filamu ya kuchangamsha iliyotolewa wakati wa Krismasi huko China, Hong Kong na Taiwan. Ikiwa ni filamu ya kizalendo, awali ilipangwa kutolewa mwezi Oktoba ili kusherehekea maadhimisho ya miaka 60 ya Jamhuri ya Watu wa China lakini ikacheleshwa mpaka mwisho wa mwaka 2009. Tofauti...
Ethiopia: Adhabu ya Kifo Ili Kuwatisha Waethiopia
Berhanu Nega, mmoja kati ya watu waliohukumiwa kifo na mahakama ya Ethiopia anasema hashangazwi na adhabu ya kifo.
Japan: Tangaza Ujumbe, Tafsiri
Mahojiano ya video [en] ya Kyo Kageura, mkuu wa mradi wa Minna no Honyaku (みんなの翻訳, Tafsiri kwa Wote) [ja], jukwaa jipya la tafsiri ambalo linazisaidia Asasi Zisizo za Kiserikali na zile Zisizo za Kibiashara kueneza ujumbe wao, shukrani kwa wafasiri wa kujitolea. Global Voices Japan ilimuuliza kuhusu changamoto za Minna...