j nambiza tungaraza · Februari, 2010

makala mpya zaidi zilizoandikwa na j nambiza tungaraza kutoka Februari, 2010

Mapinduzi Nchini Niger: Wanablogu Wapumua Pumzi ya Ahueni

Alhamisi Februari 18 mapinduzi ya kijeshi yalifanyika nchini Niger ambayo kwayo Rais Mamadou Tandja alikamatwa baada ya mapambano ya bunduki katika mji mkuu, Niamey. Miezi michache iliyopita Tandja alibadilisha katiba kinyume cha sheria ili ajiruhusu kuongoza kwa muhula wa tatu katika kile ambacho kilionekana kama dhuluma ya halaiki kwenye kura maoni. Wanablogu wanatoa mitazamo yao juu ya maendeleo haya mapya.

23 Februari 2010

Ghana: Mapendekezo ya Kuvutia Kwenye Mapitio ya Katiba

Mwaka 2008, wakati wa Uchaguzi wa rais, wagombea waliwaahidi Waghana kuwa wangeitazama tena katiba ya nchi hiyo. Jambo lililoifanya ahadi hii kuonekana kama ni ya kweli lilikuwa ni nia ya wagombea – pamoja na Rais John Atta Mills – ya kuwashirikisha Waghana katika mchakato huo wa kuitathmini katiba. Inaonekana kuwa rais ametimiza ahadi hiyo, na sasa mapendekezo mapya yanachochea mijadala ya kuvutia.

17 Februari 2010

India: Ugaidi Waikumba Pune

Mnamo majira ya saa 1:30 jioni (Februari 13, 2010) mlipuko wa bomuuliua watu 9 na kuwajeruhi wengine 57 katika mgahawa maarufu kwa watalii uliopo katika mji wa Magharibi wa Pune, India. Hisia ziko juu huku wanablogu na watumiaji wa twita wakitoa maoni.

17 Februari 2010

Haiti: Pesa Zinazotumwa na Ndugu na Jamaa Zasaidia Kabla ya Misaada Rasmi

Huku simu zikiwa zinaanza kufanya kazi tena nchini Haiti, pesa zinazotumwa na ndugu walio nje ya nchi “kwa waya” zinaanza kuwasili tena, na kusaidia ujenzi hata kule ambako mashirika ya kimataifa bado hayajafika. Pesa zinazotumwa na wanafamilia wanaoishi nje ya nchi, kwa uchache, zilikuwa kama asilimia thelathini ya Mapato ya Taifa ya Haiti kabla ya tetemeko la ardhi la Januari 12.

3 Februari 2010