makala mpya zaidi zilizoandikwa na j nambiza tungaraza kutoka Juni, 2009
Honduras: Zelaya Akamatwa na Kuondolewa Madarakani
Nchini Honduras siku ilianza na habari zinazosema kwamba Rais Mel Zelaya amekamatwa akiwa nyumbani kwake na wanajeshi wenye silaha mnamo siku ya kupigwa kura tata ya maoni. Siku chache kabla, Zelaya alimuondoa madarakani mkuu wa majeshi. Maoni yanatofautiana kutokea yale yanayosema kwamba hali iliyopo ni sawa na mapinduzi ya kijeshi mpaka yale yanayosema kuwa hii ilikuwa ndio njia pekee ya kukomesha jitihada za Zelaya za kutaka kugombea urais kwa awamu nyingine tena.
Togo Yafuta Adhabu ya Kifo
Bunge la Taifa la Togo limepiga kura ya kukomesha adhabu ya kifo na kuifanya nchi hiyo kuwa mwanachama wa 15 wa Umoja wa Nchi za Afrika kuipiga marufuku adhabu hiyo.
Iran: Video za Maandamano ya Upinzani Zazidi Kumiminika
Zaidi ya watu 100,000 waliandamana mjini Tehran Jumatatu iliyopita ili kumuunga mkono mgombea urais mwanamageuzi, Mir Hussein Mousavi pamoja na madai yake ya kuataka kubatilishwa kwa matokeo ya uchaguzi ambayo yalimtangaza rais aliye madarakani Mahmoud Ahmadinejad kama mshindi katika uchaguzi wa tarehe 12 Juni. Damu ilimwagika mwishoni mwa maandamano hayo. Watu wapatao 7 walipoteza maisha yao.
Irani: Maandamano na Ukandamizaji
Mamia ya maelfu ya Wairani mjini Tehran na katika miji mingine kadhaa wameandamana kumuunga mkono mgombea urais Mir Husein Mousavi huku wakiipuuza amri ya serikali inayokataza maandamano. Japokuwa huduma za Twita, FaceBook pamoja na YouTube zimezuiliwa kwa kuzimwa nchini Iran, Wairani wengi wamekuwa wakitumia tovuti-vivuli ili kuvizunguka vichujio vilivyowekwa na wanaripoti habari kadiri zinavyotokea. Utawala wa Irani pia umezuia huduma za jumbe za maandishi kwa kutumia simu za mkononi (SMS), kadhalika utawala huo unachuja tovuti kadhaa zinazoakisi maoni ya wanamageuzi.
Irani: Kimbunga cha Maandamano Baada Ya Uchaguzi
Maelfu ya watu waliandamana mjini Tehran, Mashdad na kwenye miji mingine mikubwa ya Irani ili kupinga ushindi wa Rais Mahmoud Ahmadinejad katika uchaguzi mkuu uliofanyika Ijumaa. Washindani wawili wanamageuzi pamoja na mashabiki wao wanasisitiza kwamba palitokea udanganyifu.
Ramani ya Ulimwengu wa Blogu za Irani Siku ya Mkesha wa Uchaguzi
John Kelly na Bruce Etling wanaelezea utafiti wao unaohusu ulimwengu wa blogu za Irani na uchaguzi katika blogu ya Intaneti na Demokrasi. Intaneti na Demokrasi ni blogu ya timu ya...
Uchaguzi Wa Irani Katika Picha
Uchaguzi wa rais nchini Irani utafanyika tarehe 12 Juni. Ni watu wanne tu kati ya watu zaidi ya 400 waliojiandikisha ambao wamepewa idhini rasmi na Baraza la Walezi kuwa wagombea katika uchaguzi. Macho makali ya wanablogu-wapiga picha yamenasa nyakati na taswira katika mitaa ya Irani ambako watu walikuwa wakiwapigia debe wagombea wanaowapenda.
Msumbiji: Shambulio Dhidi Ya Mgombea Urais
Wanablogu wa Msumbiji wanaandika kuhusu shambulio dhidi ya mwanasiasa Daviz Simango, kwenye mji wa kaskazini wa bandari ya Nacala. Pamoja na maoni kutoka kwenye ulimwengu wa blogu, chama cha Simango pia kilitumia huduma ya Twita kuandika kuhusu shambulio hilo.
Uganda: Mradi wa Katine Wawafikisha Wanakijiji Kwenye Ulimwengu wa Blogu
Inakadiriwa kuwa matumizi na uenezi wa intaneti nchini Uganda ni kwa kiwango cha asilimia sita tu, idadi ambayo inazuia sehemu kubwa ya watu kujiunga na ulimwengu wa blogu nchini Uganda au kuweza kuwasiliana na ulimwengu wa blogu duniani. Mradi wa Katine unaoendeshwa na Guardian and Observer unafanya kazi kubadilisha hali hiyo katika kijiji kimoja.