makala mpya zaidi zilizoandikwa na j nambiza tungaraza kutoka Machi, 2010
Ghana: tamasha la Twestival 2010 Mjini Accra: Shughuli Yenye Maana?
Kama uanahabari wa kijamii unabadilisha mtindo ya mawasiliano katika nchi za Magharibi, basi kwa hakika haujapungukiwa katika kufikia sehemu zinazovutia barani Afrika. . Kwa hiyo haishangazi kwamba MacJordan, wa Global Voices, anashirikiana na Rodney Quarcoo ili kulifikisha tukio hili la kuburudisha kwa watu wa Ghana.
Martinique: Uchaguzi, utata na kugomea uchaguzi
Jumapili ya tarehe 14 Machi, raia wote wa Ufaransa wakiwemo wale wa idara za ng’ambo za Ufaransa walitakiwa kupiga kura... Lakini michakato miwili ya uchaguzi katika kipindi cha miezi mitatu inaweza kuwachosha 55.55% ya wapiga kura wa Martinique ambo waliamua kubaki majumbani.
Mali: Vitambaa Vyasuka Nguzo za Uchumi na Utamaduni
Kwa kupitia video, tunaona na kujifunza kuhusu umuhimu wa utamaduni na ongezeko la kiuchumi ambalo utengenezaji vitambaa huwapa baadhi ya watu na mashirika nchini Mali. Vikundi vya wanawake, wasanii na watalii wote wananufaika na utamaduni huu wa kutia rangi vitambaa na upakaji rangi kwa kutumia matope.
Lebanoni: Wafanyakazi wa Ndani Wanaotoroka
“Mfanyakazi wa ndani anapotoroka kutoka kwenye nyumba ya mwajiri wake, kituo cha polisi hakiwezi kufanya lolote kwa sababu hakuna sheria dhidi ya wafanyakazi wa ndani wanaotoroka. Kwa hiyo ofisa wa...
Uganda: Wanafunzi Wacharuka, Kampala Yawaka Moto
Jumanne, majanga mawili tofauti yaliikumba Kampala, mji mkuu wa Uganda: wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Makerere walifanya ghasia baada ya wanafunzi wenzao wawili kupigwa risasi. Na makaburi ya Kasubi, ambayo ni sehemu ya Urithi wa Dunia ya UNESCO na eneo la kaburi la mfalme wa moja ya makabila makubwa zaidi ya Uganda, liliteketea kwa moto.
Afrika Kusini: Ubaguzi wa Julius Malema
Wakati tabia za Rais Jacob Zuma zimekuwa zikizua mijadala mikali na yenye uhai katika ulimwengu wa blogu wa Afrika Kusini, hivi sasa ni mwanasiasa mwenye utata ambaye pia ni rais wa Umoja wa Vijana wa ANC, Julius malema ambaye anatengeneza vichwa vya habari. Hivi karibuni, aliwaongoza wanafunzi katika kuimba wimbo wa zamani wa kupinga ubaguzi wa rangi unaoitwa Ua Kaburu.
Thailand: Utulivu Kabla ya Kimbunga?
Maandanmano ya kuipinga serikali ya Machi 12 yalimalika salama huku kundi la Mashati Mekundu likiapa kurejea tena mitaani mwishoni maw juma hili ili kuendelea kushinikiza kuvunjwa kwa bunge na kuitisha uchaguzi mkuu. Wanablogu na watumiaji wa Twita wanatoa maoni yao.
Moroko: Wafanyakazi wa Shirika la Misaada La Kikristu Wafukuzwa
Wiki iliyopita, wafanyakazi 20 wa Kijiji cha Matumaini, makazi madogo ya yatima katika mji mdogo wa Moroko vijijini, waliondolewa (walifukuzwa) nchini bila onyo, kwa madai ya kuhubiri dini.
Sudani: Je, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Itafanya Kazi?
Jarida la The Financial Times liliripoti hivi karibuni kuwa mpango wa mamilioni ya dola wa Benki ya Dunia wa kusambaza kompyuta na upatikanaji wa Intaneti huko Juba, mji mkuu wa Sudani ya Kusini, umeshindwa. habari hizi zinazua swali: kelele zinazoambatana na teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) zina uhalali?
Chile: Tetemeko la Ardhi Lafichua Ukosefu wa usawa Katika Jamii
Ukiukwaji sheria kulikojitokeza baada ya tetemeko la ardhi la Februari 27 nchini Chile kumezua mjadala wa kitaifa kuhusu kutokuwepo kwa usawa wa kijamii na kiuchumi nchini.