makala mpya zaidi zilizoandikwa na j nambiza tungaraza kutoka Disemba, 2009
Je, China Iliharibu Makubaliano ya Copenhagen?
Uln alijaribu kuchambua ni nini kilichotokea Copenhagen na kuhoji kwa nini nchi zinazoendelea hazikusaini baina yao wenyewe makubaliano ya kupunguza utokaji wa gesi ya ukaa. Inside-Out China ametafsiri taarifa inayosimulia...
Msumbiji: Je, ni Lugha Ngapi Zinazungumzwa Nchini?
Kuna lugha 20 zinazozungumzwa nchini Msumbiji, kwa mujibu wa tovuti ya serikali, zaidi ya lugha ya serikali ya Kireno. Carlos Serra [pt] anajiuliza kama kuna lugha nyingine zaidi, kwa mujibu...
Malawi: Wanablogu Wajadili Matetemeko ya Ardhi 30 Katika Wiki 3
Katika kile ambacho baadhi ya wataalamu wa miamba wamekieleza kama matukio ya nadra, Wilaya ya Kaskazini ya Karinga nchini Malawi imeshuhudia jumla ya matetemeko ya ardhi 30 katika wiki tatu zilizopita ambayo yamesababisha vifo 5, zaidi ya watu 200 kujeruhiwa na zaidi ya watu 3,000 kupoteza makazi. Wanablogu wamekuwa wepesi kushirikiana maoni.
Global Voices Yaingia Ubia na Google Katika Tuzo ya Uhuru wa Kujieleza
Mapendekezo kwa ajili ya Tuzo ya Kuvunja Mipaka yatafunguliwa leo (Disemba 29, 2009), hii ni tuzo mpya aliyoundwa na Google pamoja na Global Voices ili kuienzi miradi ya kwenye mtandao wa intaneti iliyoanzishwa na watu au vikundi ambavyo vinaonyesha ujasiri, ari na uwezo katika kutumia intaneti ili kukuza uhuru wa kujieleza.
Malaysia: Mtetezi wa Uhuru wa Vyombo vya Habari Amshtaki Mwanablogu
Mwanahabari-mwanablogu mkongwe anashtakiwa katika kesi ya madai na mwanasiasa anayejulikana kwa kutetea uhuru wa habari nchini Malaysia. Angalia maoni ya wanablogu wa Malaysia.
Rwanda: Video za Wanaojitolea
Mfululizo wa video zilizopakiwa na mtumiaji kdarpa kwenye YouTube, zinaonyesha wafanyakazi wa kujitolea na watu waliokutana nao wakiwa safarini nchini Rwanda ambapo walifanya kazi na jamii za sehemu hiyo.
Uganda: Rais Kuzuia Muswada Unaopinga Ushoga
Muswada Unaopinga Ushoga wa 2009 uliopendekezwa nchini Uganda bado unasubiri uamuzi wa mwisho utakaotolewa na bunge la nchi hiyo, lakini gazeti la Daily Monitor lilitaarifu Jumatano kuwa Rais Yoweri Museveni ameihakikishia Idara ya Mambo ya Nje ya Marekani nia yake ya kuukwamisha muswada huo
Ecuador: Serikali Yaifungia Idhaa ya Televisheni ya Teleamazonas
Serikali ya Ecuador iliiondoa idhaa ya televisheni ya teleamazonas kwa masaa 72 kwa kusambaza habari za uongo. Wakosoaji wanaona kuwa hatua hii ni tishio kwa uhuru wa kujieleza.
Podikasti: Mahojiano na Sudanese Drima
Sudanese Drima ni jina la bandia la mwandishi wa Kisudani wa Global Voices anayeishi nchini Malaysia. Katika mahojiano haya ya dakika kumi tunajadili jinsi uanahabari wa kijamii unavyoathiri Uislamu, mgogoro wa dafur, na masuala ya nafsi ya Uafrika-Uarabu katika Asia ya Kusini Mashariki.
Iran: Maandamano Tehran
Hii ni video inayoonyesha waandamanaji huko Manzarieh na Nyavaran mjini tehran wakiimba kauli mbiu dhidi ya utawala wa Kiislamu Jumamosi.