j nambiza tungaraza

Anwani ya Barua Pepe j nambiza tungaraza

makala mpya zaidi zilizoandikwa na j nambiza tungaraza

Tanzania: Mwigizaji Nyota wa Filamu, Steven Kanumba, Afariki Dunia

Tanzania ilimuaga mmoja wa wasanii wake maarufu na nyota wa tasnia ya filamu, Steven Kanumba, kwa maziko yaliyogubikwa na majonzi mazito mnamo tarehe 11 Aprili 2012. Alifariki alfajiri ya Jumamosi, akiwa na umri wa miaka 28, baada ya kile kilichodaiwa kuwa ugomvi wa kimapenzi na rafiki yake wa kike aitwaye Elizabeth Michael kwa jina maarufu “Lulu”.

13 Aprili 2012

Uganda: Polisi Wawanyunyizia Waandamanaji Rangi ya Waridi

Polisi wa Uganda wameikabili kampeni inayoendelea kwa mwezi mmoja sasa ya Kutembea Kwenda Kazini kwa kuwanyunyuzia waandamanaji moshi wa machozi na risasi sa moto. Wakati wa maandamano siku ya Jumanne, walitumia mbinu mpya, ya kuwashambula waandamanaji waliokuwa wakijaribu kuandamana kuelekea viwanja vya katiba katikati ya jiji la Kampala kwa maji yaliyochanganywa na uji wa rangi ya waridi.

18 Mei 2011

Singapore: Wanablogu Waikosoa Ilani ya PAP

Chama kinachotawala Singapore, People’s Action Party (PAP), kilitoa ilani yake ya uchaguzi tarehe 17 aprili, 2011, ambayo mara moja ilikosolewa na wanablogu wengi kwa “kutokuwa wazi”. PAP tayari kimekuwa madarakani kwa miongo mitano. Uchaguzi mkuu nchini humo umefanyika tarehe 7 Mei.

12 Mei 2011

Senegal: Harakati za “Imetosha Sasa Basi”: Kwanza Kwenye Mtandao, Na Sasa Ikulu

Wakati vuguvugu la mapinduzi likiendelea Uarabuni, matukio kadhaa ya vijana wenye hasira yamezuka katika tovuti za Senegal. Tangu mwanzoni mwa mwezi wa tatu, uanaharakati huo umeachana na ulimwengu wa mtandao na kundi linalojiita “Y'en a marre” (Imetosha Sasa Basi) sasa limegeuka na kuwa alama ya vuguvugu la upinzani. Founded in January 2011, Y’en a marre arose from frustration built up during power cuts that brought Senegal to a standstill. The group hails from the Dakar suburbs and is led by several local rappers, including Fou Malad, Thiat (from the group Keur Gui) and Matador.

10 Mei 2011