makala mpya zaidi zilizoandikwa na j nambiza tungaraza kutoka Aprili, 2011
Kenya: Uanahabari wa kiraia wa Mtandao wa Habari wa Kibera
Vijana wa Kibera, Kenya, kitongoji ambacho kinajulikana kwa baadhi kama eneo kubwa la hovyo zaidi ya yote barani Afrika, wamedhamiria kuonesha sura nyingine ya mahali wanapoishi. Huku wakiwa na kamera mkononi, wanavinjari mitaa kutafuta habari kuinesha dunia jinsi Kibera inavyojiona yenyewe.
Naijeria Yapiga Kura 2011: Maoni kutoka kwenye Uchaguzi
Wanaijeria walipiga kura jana katika uchaguzi wa tatu wa rais tangu taifa hilo lilipoingia kwenye utawala wa kiraia mwaka 1999. Mpaka sasa, uchaguzi huo umeelezwa na wengi kuwa ulikuwa wa mafanikio, huku kukiwa na taarifa za ghasia za hapa na pale pamoja na hitilafu za upigaji kura. Vyanzo vya habari vimeripoti kuwa watu wengi walijitokeza, foleni zenye kufuata utaratibu, na wapiga kura kusubiri hadi uchaguzi utakapomalizika ili kuhakikisha kwamba kura zao zimehesabiwa. Wanablogu wanajadili.
Côte d'Ivoire: Kuanguka kwa Laurent Gbagbo
Laurent Gbagbo alikamatwa katika makazi yake ya Cocody, pamoja na mkewe, Simone, na msafara wa watu wa karibu. Miezi mitano baada ya kukataa kukabidhi madaraka kwa rais anayetambuliwa kimataifa kama rais mpya wa Côte d'Ivoire, Alassane Ouattara, mgogoro nchini humo hivi sasa unaelekea kufikia hitimisho.Mtiririko wa matukio yaliyopelekea kukamatwa kwa Gbagbo yaliorodheshwa kwa kina kwa njia ya video za kwenye mtandao ambazo zilitolewa maoni kwenye mtandao.
Naijeria: Maonesho ya Picha za Kampeni ya Urais
George Esiri alifuatilia kampeni za kugombea urais za chama cha PDP huko Naijeria. Maonesho ya picha alizopiga yalizinduliwa jana katika Kituo cha Yar'Adua.
Côte d'Ivoire: Televisheni ya Taifa RTI Inawezekana kuwa Inatangaza Kutokea Kwenye Gari la Matangazo
Kama vile alivyoelezea Julie Owono , ni vigumu kupembua mapambano ya kudhibiti vyombo vya habari vya Pwani ya Pembe (Cote d'Ivoire). Taarifa kutoka Waandishi Wasio na Mipaka inaashiria kuwa RTI...