makala mpya zaidi zilizoandikwa na j nambiza tungaraza kutoka Januari, 2010
Rais wa Malawi kutangaza rasmi penzi lake siku ya Valentine
Wamalawi wanatafakari taarifa kuwa mnamo tarehe 1 Mei, rais wa nchi Dkt. Bingu wa Mutharika anatarajiwa kumuoa waziri wa zamani wa utalii Callister Moyo. Harusi hiyo itatanguliwa na sherehe za kitamaduni za uchumba wakati wa siku ya wapendanao ya Valentino tarehe 14 Februari. Wanabloga wachache wamemtakia heri rais katika mapenzi mapya aliyoyapata baada ya kifo cha mkewe Ethel miaka mitatu iliyopita.
Naijeria: Uzoma Okere ashinda kesi dhidi ya jeshi
Nigerian curiosity anaandika kuhusu kesi ya Uzoma Okere huko Naijeria: “Uzoma Okere ni msichana wa Kinaijeria ambaye kipigo alichopata kutoka kwa maafisa wa jeshi kiliondokea kuwa video iliyosambazwa sana na...
Eritrea: Utawala Ulio Madarakani Uondelewe Haraka
Kwa mujibu wa Mohammed Hagos, mradi wa demokrasi katika Eritrea unapaswa uanze kwa kuuondoa madarakani utawala uliopo sasa: “Kikwazo kinachowazuia watu wa Eritrea kujieleza ni utawala wa Issayas. Njia ya...
Philippines: “Muswada wa Mkataba wa Ndoa Jadidifu”
Kikundi kimoja cha masuala maalum ya jamii nchini Philippines kinataka kuwasilisha sheria ambayo itaufanya mkataba wa ndoa kuwa na nguvu kwa miaka kumi tu. Pendekezo hilo la kipekee limezua mjadala mkali kwenye ulimwengu wa blogu.
Haiti: Kituo Cha Habari Chazinduliwa Kwa Ajili Ya Uanahabari wa Haiti
Réseau Citadelle anatangaza kuzinduliwa kwa Kituo Cha Habari, mradi unaotoka kwa Wanahabari Wasio Na Mipaka pamoja na Quebecor, wenye lengo la kuwezesha kazi za wanahabari wa ndani na wa nje...
Lebanoni: Watu 90 Wanahofiwa Kufariki Baada ya Ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia Kuanguka Baharini
Rambirambi zilimiminika kwenye Twita baada ya ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia kuanguka kwenye (bahari ya) Mediterani dakika chache baaday ya kupaa ikitokea Beirut, Lebanoni. Watu wote 90 waliokuwemo wanahofiwa kuwa wamekufa baada ya ndege hiyo kushika moto katika kimbunga cha radi na kuangukia baharini.
China: Tangazo la Google Kusahihisha Uvumi Limezua Utabiri Mwingine
Tangazo la hivi karibuni la Google.cn linasema kuwa uvumi kuhusu kujitoa kwake ni uvumi tu. Hata hivyo, utabiri zaidi ulijitokeza, ukiuliza iwapo uamuzi wa Google unalenga kuficha kushindwa kwake kibiashara, au unalenga kutumikia maslahi ya kisiasa.
Colombia: Ugumu wa Kutofautisha Wazuri na Wabaya
Kwa kupitia upigaji video wa kiraia, asasi tofauti nchini Colombia zinatoa mitazamo yao kuhusu uhalifu, unyama na migogoro inayohusisha matumizi ya silaha, ambayo ni vigumu kuwatofautisha watu wazuri kutoka kwa wabaya.
Kenya: Kiswahili Kuwa Somo La Kuchagua
Bunmi anaandika kuhusu uamuzi wa kulifanya somo la Kiswahili kuwa la kuchagua nchini Kenya: “Somo hili halitakuwa tena na mtihani wa lazima katika mtihani wa taifa wa darasa la nane…”
Marekani: Dkt. Martin Luther King, Jr. Akumbukwa
Martin Luther King Jr. alizaliwa tarehe 15 Januari, 1929 na akawa mmoja wa wasemaji na watetezi wakuu wa Harakati za Haki za Kiraia huko Marekani. Nchini Marekani, anaenziwa kwa sikukuu ya taifa, inayoadhimishwa kila mwaka siku ya Jumatatu ya tatu ya mwezi Januari. Leo, wanablogu wengi nchini Marekani wanaadhimisha kumbukumbu yake kwa kuandika makala za kumuenzi, huku wakiungalisha urithi wake wa masuala ya haki za jamii na masuala ya leo, wakionyesha wazi kuwa miaka 42 baada ya kuuwawa kwa King, maneno yake bado yana maana.