makala mpya zaidi zilizoandikwa na j nambiza tungaraza kutoka Aprili, 2012
Tanzania: Mwigizaji Nyota wa Filamu, Steven Kanumba, Afariki Dunia
Tanzania ilimuaga mmoja wa wasanii wake maarufu na nyota wa tasnia ya filamu, Steven Kanumba, kwa maziko yaliyogubikwa na majonzi mazito mnamo tarehe 11 Aprili 2012. Alifariki alfajiri ya Jumamosi, akiwa na umri wa miaka 28, baada ya kile kilichodaiwa kuwa ugomvi wa kimapenzi na rafiki yake wa kike aitwaye Elizabeth Michael kwa jina maarufu “Lulu”.
Malawi: Maoni ya Mtandaoni Kuhusu Kifo cha Mutharika
Victor Kaonga anaangalia maoni ya mtandaoni kufuatia habari za kifo cha Bingu wa Mutharika. Mutharika alikuwa rais wa tatu wa Malawi. Alifariki baada ya mshtuko wa moyo asubuhi ya Alhamisi. Hii ni mara ya kwanza kwa Malawi kumzika rais aliyefariki akiwa madarakani.