Habari kuhusu Saudi Arabia
Dunia ya Uarabu: “Acheni Kulia Juu Sudani”
Kura ya maoni kwa ajili ya uhuru wa Sudani ya Kusini leo imeiweka nchi hiyo kwenye uangalizi wa karibu miongoni mwa watumiaji wa twita wa Kiarabu. Kuanzia Saudi Arabia mpaka Palestina, watumiaji Twita wa Kiarabu wanajadiliana kuhusu mshikamano, kugawanyika na rasili mali za Sudani.
Mashariki ya Kati: Mawasiliano ya Siri Ambayo Sio Siri ya Ubalozi wa Marekani
Wakati vyombo vya habari vikuu Uarabuni vimeyapokea kwa bega baridi mawasiliano ya siri ya Balozi za Kimarekani, wanablogu na watumiaji wa Twita kutoka Mashariki ya Kati walipata habari zinazohitajika sana kwa uchambuzi.
Saudia Arabia: Ambako Kuiga Kazi Kinyume cha Haki Miliki ni Kosa la Jinai
Wanablogu wa Kisaudia wanaungana ili kumuunga mkono mwanablogu mwenzao anayelituhumu gazeti moja kuwa limetumia picha na kuzinakili kutoka mwenye blogu yake bila ruhusa.
Nchi za Kiarabu: Homa ya Mafua ya Nguruwe Yaendelea
Homa ya mafua ya nguruwe au H1N1 bado inatawala vichwa vya habari vya magazeti katika nchi za Kiarabu kwani wagonjwa wapya wanaendelea kugunduliwa na mamlaka za afya na kutangazwa katika vyombo vya habari kila siku. Huu ni muhtasari wa yale wanayoongea wanablogu huko Bahrain, Jordan, Misri na Syria.
Saudi Arabia: Je, mafua ya nguruwe yatatishia Hija?
Kila mwaka mamilioni ya Waislamu hukusanyikia Maka kuhiji, moja ya nguzo tano za Uislamu. Je, msimu wa hija ya mwaka huu utatishiwa na homa ya mafua ya nguruwe? Wanablogu wanayo maoni ya kusema.
Mashariki ya Kati: Vikwazo kama Silaha ya Kisiasa
Watu wengi wa Mashariki ya Kati wamesusia bidhaa za Israeli na Marekani kama jibu la mashambulizi ya Israeli huko Gaza. Tarek Amr anapitia yale wanablogu wanayosema kuhusu suala hili.
Saudi Arabia: Kina Mama Huru
WAKATI kukiwa hakuna shaka kwamba kuna vizuizi kwa wanawake waishio Saudi Arabia, havifanani na taswira iliyojengwa na wageni dhidi ya taifa hilo. Katika makala hii tunao ushauri kwa wakina mama wanaotaka kutembelea jiji la Jeddah wakiwa peke yao, kuna muhtasari wa hoteli za kina mama pekee jijini Riyadh, na wito kwa wageni wote wanajihisi kuzungumza kwa niana ya kina mama wanaokandamizwa wa Saudia.