Habari kuhusu Aljeria

Uarabuni: Sera ya Romney kwa Mashariki ya Kati Yaibua Mjadala

Hotuba ya Mgombea urais wa Marekani kupitia chama cha Republican Bw. Mitt Romney iliyoelezea sera yake ya nje imeibua mjadala mzito miongoni mwa raia wa mtandaoni leo hasa wale watokao katika nchi za ki-Arabuni. Twiti zinazohoji sera ya mambo ya nje ya Marekani kwa Mashariki ya Kati ziliendelea wakati ambao Romney, anayepeperusha bendera ya chama cha Republican, alipozungumza katika Chuo cha Jeshi cha Virginia. Endapo atachaguliwa, Romney ameahidi kuwa na sera rafiki za mambo ya nje, tofauti na mwelekeo usiotabirika wa sera za Obama wakati huu ambapo mabadiliko ya kisiasa yanaendelea kulikumba eneo la Mashariki ya Kati.

8 Oktoba 2012

Misri na Aljeria: Pambano la Twita

Katika sehemu nyingi duniani, hakuna linalounganisha zaidi – au wakati mwingine kutenganisha – zaidi ya pambano la mpira wa miguu. Washabiki wa Misri na Aljeria, katika ulimwengu wote wa Waarabu na zaidi, walilidhihirisha hilo Jumamosi hii wakati timu zao zilipokwenda sambamba wakati wa kuwania kuingia fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini.

16 Novemba 2009