Habari kuhusu Aljeria
Mwanablogu wa Algeria Merzoug Touati Anaweza Kutumikia Jela Miaka 25 Kwa Kufanya Mahojiano na Afisa wa Israel Kupitia Mtandao wa You Tube

Mahojiano yake yanahusu tuhuma za serikali ya Algeria kwamba mataifa ya nje yanachochea maandamano ya kupinga hatua iliyochukuliwa na serikali ya kubana matumizi. Mwanablogu Merzoug Touati anakabiliwa na makosa ya "kutoa taarifa za kiintelijensia kwa afisa wa mataifa ya kigeni."
Mahakama Nchini Algeria Yaonesha Msimamo dhidi ya Mashtaka ya Mwanaharakati Aliyefungwa kwa Kutusi Uislamu Kupitia Facebook

Pamoja na kuwa adhabu yake imepunguzwa kwa miaka miwili, Bouhafs ataendelea kutumikia adhabu yake gerezani kwa kutumia uhuru wake wa kujieleza.
Mtazamo wa Tamasha la Kwanza la WanaBlogu na Vilogu wa Barani Afrika Lililofanyika Huko Dakar, Senegal
Kwa siku mbili, wanablogu na wanavilogu maarufu barani Afrika, wakiambatana na wadau kadhaa wa teknolojia barani Afrika walikuwa na majadiliano ya namna ya kuboresha kazi zao
Picha za Mabaki ya Ndege ya Shirika la Algeria AH5017 Nchini Mali Yaonyesha Ghasia, Kuanguka kwa Ghafla
VERY FIRST images of #AH5017 #AirAlgerie trickling out, via @AirLiveNet http://t.co/4pKox7rgjn pic.twitter.com/rngGTv7Rbs — Jason Morrell (@CNNJason) July 25, 2014 PICHA ZA KWANZA za ndege ya AH5017 ya Shirika la Ndege...
Hivi Ndivyo Waandishi wa Kifaransa wa Global Voices Wajivyojipanga Kusoma Kiangazi Hiki
Je, unahitaji kitabu cha kujisomea? Hapa kuna orodha ya kusoma iliyopendekezwa na waandishi wa Kifaransa kwa familia ya GV.
Hadithi ya Wakimbizi wa Njaa kutoka Niger katika Algeria Mashariki
Katika wiki chache zilizopita, mamia ya wahamiaji mwa Jangwa la Sahara kutoka Mali au Niger wamehamia miji ya Algeria katika mpaka wa Mashariki. Liberté Algérie anasimulia hadithi ya wale ambao...
Mchora Katuni wa Algeria Ahukumiwa Kifungo cha Miezi 18 Jela kwa Kumdhihaki Rais
Djamel Ghanem anakabiliwa na kifungo cha jela kwa kuchora katuni inayoufananisha mpango wa Rais wa Aljeria Abdelaziz Bouteflika wa awamu ya nne na nepi ya mtoto. Katuni hiyo, hata hivyo haikuwahi kuchapishwa
Uarabuni: Sera ya Romney kwa Mashariki ya Kati Yaibua Mjadala
Hotuba ya Mgombea urais wa Marekani kupitia chama cha Republican Bw. Mitt Romney iliyoelezea sera yake ya nje imeibua mjadala mzito miongoni mwa raia wa mtandaoni leo hasa wale watokao katika nchi za ki-Arabuni. Twiti zinazohoji sera ya mambo ya nje ya Marekani kwa Mashariki ya Kati ziliendelea wakati ambao Romney, anayepeperusha bendera ya chama cha Republican, alipozungumza katika Chuo cha Jeshi cha Virginia. Endapo atachaguliwa, Romney ameahidi kuwa na sera rafiki za mambo ya nje, tofauti na mwelekeo usiotabirika wa sera za Obama wakati huu ambapo mabadiliko ya kisiasa yanaendelea kulikumba eneo la Mashariki ya Kati.
Moroko: Kupinga Mateso Sehemu Moja; Kupinga Mateso Kila Sehemu
Wanablogu wa Moroko wamekuwa wakionyesha kukasirishwa kwao juu ya tabia ya kutojali ya vyombo vya habari vikubwa na unafiki wa serikali yao kufuatia kifo cha kijana wa KiMoroko mikononi mwa wawakilishi wa serikali.
Misri na Aljeria: Pambano la Twita
Katika sehemu nyingi duniani, hakuna linalounganisha zaidi – au wakati mwingine kutenganisha – zaidi ya pambano la mpira wa miguu. Washabiki wa Misri na Aljeria, katika ulimwengu wote wa Waarabu na zaidi, walilidhihirisha hilo Jumamosi hii wakati timu zao zilipokwenda sambamba wakati wa kuwania kuingia fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini.