Habari kuhusu Iran
Iran:Raia wa Mtandaoni Wanane Wakamatwa
Mamlaka ya Iran ilitangaza kuwa raia wa mtandaoni wanane ikiwa ni pamoja na mwanamke mmoja walikamatwa katika Rafsanjan, katika Mkoa wa Kerman, kwa madai ya “kutusi utakatifu wa Kiislamu na maadili”.
Je, Kutakuwa na Fungate kwa Marekani na Irani?
Raia wa Iran hawakubaliani ikiwa mahusiano mazuri yaliyoashiriwa na tukio la kupigiana simu kati ya Marais Obama na Rouhani ni jambo jema.
Iran: “Mauaji” ya Wapinzani wa Iran 52 Wasiokuwa na Silaha
Vikosi vya usalama vya Iraq vilifanya “mauaji” ya wapinzani wa Iran wapatao 52 ambao hata hivyo hawakuwa na silaha asubuhi ya Jumapili ndani ya kambi yao kaskazini mwa Baghdad, mujahedeen-e-Khalq, wafungwa wa Iran walisema. Netizens in Balatarin, tovuti maarufu ya kusambaza habarii, iliweka picha kadhaa, filamu na posti kuhusiana na shambulio...
Iran: Mwanablogu Aliyefungwa Jela Afanya Mgomo wa Kutokula
Hossein Ronaghi Malki mwanablogu anayetumikia kifungo cha miaka 15 jela alianza mgomo wake wa kutokula kuanzia wiki iliyopita. Kwenye mtandao wa Facebook kampeni imeanzishwa yenye lengo la kummwuunga mkono.
Iran: Waziri Mpya wa Kigeni Yupo Kwenye Mtandao wa Facebook
Waziri mpya wa Uhusiano wa Kimataifa wa Iran Mohammad Javad Zarif ana ukurasa wa Facebook ambapo huutumia kujibu maswali. Anasema “Mimi na watoto wangu huuhuisha (kuweka habari mpya) ukurasa huu.” Ukurasa huo una zaidi ya wafuatialiaji 79,854 walioupenda (wakati wa kutafsiriwa kwa posti hii). Mtandao wa Facebook hudhibitiwa nchini Iran lakini ndio...
Iran: Je, Ufunguo wa Rais Mpya “Utafungua” Tatizo Lolote?
Alama ya kampeni za Rouhani ilikuwa ni Ufunguo. Kwa sasa, raia wa mtandaoni wa Iran wanajadili kama Rouhani ataweza kufungua kila kifungio.
Wanaharakati 36 wa Azeri Wakamatwa nchini Iran
Wanaharakati thelathini na sita wa Azeri akiwamo mwanablogu mmoja, Kiaksar, walikamatwa siku ya Alhamisi, 27 Juni katika eneo la Urmia. Vikosi vya usalama viliwaachilia huru wanaharakati hao 300 baada ya kuwahoji kwa masaa kadhaa.
‘Sauti za Iran’ Mradi Unaowapa Sauti Raia Waishio Vijijini
Sauti za Iran ni mradi ulioundwa kwa kutumia mafanikio ya mradi wa Ushahidi. Sauti za Iran inakusudia kuripoti habari kuhusu miji midogo na vijiji vya Iran na vile vile kukusanya maombi na matatizo ya wananchi na kuyatuma kwa serikali na wabunge.
Iran: Utani Kuhusu Mdahalo wa Urais
Raia wa mtandaoni kadhaa walitwiti kuhusu mjadala wa pili wa rais na waliwakejeli wagombea. Potkin Azarmehr alitwiti “Wagombea urais wanaweza kuombwa kucheza muziki.”
Irani: Je, Dola Inamwogopa Msichana wa Miaka 13?
Kuwapiga watu marufuku kusafiri nje ya nchi yamekuwa mazoea ya serikali ya Irani kwa makusudi ya kuwaghasi wanaharakati wa asasi za kisiasa na zile za kiraia kwa miaka mingi. Lakini, mahakama ya usalama iliwasha moto upya kwa kumpiga marufuku kusafiri nje ya nchi mume wa mwanasheria wa haki za binadamu aliyefungwa Nasrin Sotoudeh pamoja na binti yao mwenye umri wa miaka kumi na mitatu, Mehraveh Khandan. Nasrin Stoudeh amehukumiwa miaka kumi na moja gerezani.