Habari kutoka Muhtasari wa Habari na Tanzania
Tunayoyajua na Tusiyoyajua Baada ya Jaribio la Mapinduzi Nchini Burundi
Celebration and jubilation near Presidential offices in Bujumbura after the overthrow of Nkurunziza. #BurundiCoup pic.twitter.com/WhJzXKfS69 — Robert ALAI (@RobertAlai) May 13, 2015 Shangwe na vifijo karibu na ikulu ya Rais nchini Bujumbura baada ya kupinduliwa kwa Nkurunzisa. Kufuatia nia ya kugombea urais kwa kipindi cha tatu ya Rais wa Burundi...
2015 Mwaka wa Kufanyika Chaguzi Huru na Haki Barani Afrika
Wekesa Sylvanus anataraji kwamba 2015 utakuwa mwaka wa chaguzi huru na haki barani Afrika: https://wekesasylvanus.wordpress.com/2015/02/18/will-2015-be-a-year-of-free-and-fair-elections-in-africa/ Tangu kurejeshwa kwa mfumo wa demokrasia ya vyama vingi barani Afrika, ushindani nyakati za uchaguzi umekuwa suala la kufa na kupona kwenye nchi nyingi za ki-Afrika. Chaguzi barani Afrika ni suala lenye hatari zake na...
Mkusanyiko wa Makala za Kuvuliwa Madaraka kwa Mbunge Maarufu Nchini Tanzania
Ben Taylor aweka mkusanyiko wa makala zinazohusiana na kuvuliwa madaraka kwa Zitto Kabwe,mbunge maarufu na kijana wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, Chadema. Zitto: […] alivuliwa nyadhifa zote rasmi na viongozi wakuu wa chama mapema siku ya ijumaa asubuhi. Zitto Kabwe hatakuwa tena Naibu katibu Mkuu wa chama wala...
Fuatilia SafariYaGariAfrika Mtandaoni
Kikundi cha watengenezaji na wabunifu wa teknolojia kutoka Ulaya ambao wanadadisi ukuaji wa vituo vya teknolojia barani Afrika wanaendelea na safari yao ya gari barani humu. Tazama blogu yao au Tumblr na ufuatilie mjadala kuhusu safari yao kwenye mtandao wa Twita.
Serikali ya Tanzania Yafunga Magazeti Mawili
Serikali jana (terehe 27 Septemba, 2013) ilitangaza kuyafungia magazeti ya Mwananchi na Mtanzania kutokana na kuandika habari na makala zilizoelezwa zina nia ya kusababisha wananchi wakose imani kwa vyombo vya dola na kuhatarisha amani. Taarifa ya kufungiwa magazeti hayo ilisema; Gazeti la MWANANCHI limefungiwa kutochapishwa kwa siku kumi na nne(14)...
Tanzania: Uchaguzi Mdogo wa Madiwani Arusha Waipa CHADEMA Ushindi
Uchaguzi mdogo wa Madiwani Jijini Arusha umefanyika kwa amani leo Jumapili Julai 14. Mtandao maarufu wa Jamii Forums uliripoti yanayoendelea Arusha wakati wote na baada ya uchaguzi. Blogu ya Wavuti imeweka matokeo ya uchaguzi huo pamoja na picha mbalimbali za uchaguzi: Huku Tume ya Uchaguzi ikisubiriwa kuwatangaza rasmi washindi, taarifa...
Rais Obama Kuitembelea Tanzania
Rais wa kwanza wa Marekani mwenye asili ya Afrika, Barack Obama anatarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam kesho alasiri kwa ziara ya kiserikali. Blogu ya Swahili Time imeweka ratiba ya ziara hiyo ya siku mbili. Issa Michuzi aliweka video inayomwonesha Rais Kikwete wa Tanzania akizungumzia ziara hiyo.
Mfululizo wa Tamthilia ya Runinga ya Nchini Tanzania
The Team Tanzania (Timu Tanzania) ni mfululizo wa Tamthilia ya Runinga yenye kuzungumzia: […] Bi. Wito, mwalimu mahiri wa somo la uraia, anaigeuza kabisa mitazamo ya vijana makinda watatu anapowauliza maswali mazito mfano “Wewe ni nani”? vijana wale wenye umri wa miaka 16, waliofahamiana vyema tangu wakikua. Katika kuingia katika...
Michoro ya Dar: Sanaa kwa Maendeleo Endelevu
Dar Sketches (Michoro ya Dar) ni sehemu ya mradi unaoanzia ngazi ya Mtaa jijini Dar Es Salaam, Tanzania ulioanzishwa na msanii na mchoraji Sarah Markes: Ni katika kuenzi urithi wa kitamaduni na wa sanaa ya ubunifu wa majengo kwa jiji la Dar Es Salaam sambamba na juhudi za kukuza uelewa...
Tanzania: Ghorofa Laporomoka jijini Dar Es Salaam
Pernille anaweka picha mtandaoni zinazoonyesha ghorofa lililoporomoka jijini Dar Es Salaam, Tanzania siku ya Ijumaa, 29 Machi 20013: “Karibu kabisa na jengo hilo kuna uwanja wa kandanda unaotumiwa na watoto. Zaidi ya watu 60, pamoja na watoto, wanaripotiwa kupotea kwa mujibu wa kituo cha televisheni cha ITV. Hakuna kauli rasmi...