· Aprili, 2011

Habari kuhusu Sheria kutoka Aprili, 2011

Misri: Mubarak awekwa Kizuizini

Miezi michache tu iliyopita, raia wengi wa Misri walitamani sana kumwona aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Rais Mubarak, akitupwa jela, hata hivyo, pengine ni wachache miongoni mwao waliofikiri kwa uhakika kabisa kwamba siku moja jambo hili lingetimia. Hata hivyo, mnamo Jumatano ya tarehe 13 Aprili, 2011, raia wa Misri waliamka na mapema asubuhi ya siku hiyohiyo kukutana na habari zinazohusu Mubaraka kutupwa kizuizini. Hapa chini tunawaletea jinsi habari hizi zilivyopokelewa katika ulimwengu wa uandishi wa habari wa Kijmii miongoni mwa Wamisri.

22 Aprili 2011

Wanablogu wa Kenya Waunda Umoja; BAKE

Mnamo tarehe 25 Machi, wanablogu kadhaa wa Kenya walifanya mkutano katika mji mkuu wa nchi hiyo, Nairobi, mkutano uliitishwa na BAKE (Bloggers Association KEnya). Huo ulikuwa mkutano wa 4 uliotokana na msukumo wa wanablogu wakongwe wa Kenya.

4 Aprili 2011