· Februari, 2010

Habari kuhusu Sheria kutoka Februari, 2010

Nijeria: Baada ya miezi miwili bila uongozi, kaimu Rais mpya

Baada ya wiki za mivutano ya kisiasa, Baraza la Seneti lilimthibitisha Goodluck Jonathan kama kaimu Rais. Wengi kwenye ulimwengu wa blogu waliliona tukio hilo kama sababu ya kusherehekea… lakini wengine waliliona kama jambo la kutia hofu, wakieleza kwamba japokuwa kutwaa madaraka kwa Jonathan kunaweza kuwa ni ulazima wa kisiasa, kutwaa huko hakujaruhusiwa wazi na katiba ya Naijeria.

Haiti: Kwa Nini Habari Zote Hizi Kuhusu Yatima?

  24 Februari 2010

Mwezi mmoja baada ya tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa poiti saba kuangamiza sehemu kubwa ya Haiti ya kusini, mustakabali wa watoto, na hasa hasa yatima, umekuwa ni habari kubwa katika kona mbalimbali. Lakini sauti za Wahaiti kwenye mada husika zimekuwa chache...

India: Ugaidi Waikumba Pune

  17 Februari 2010

Mnamo majira ya saa 1:30 jioni (Februari 13, 2010) mlipuko wa bomuuliua watu 9 na kuwajeruhi wengine 57 katika mgahawa maarufu kwa watalii uliopo katika mji wa Magharibi wa Pune, India. Hisia ziko juu huku wanablogu na watumiaji wa twita wakitoa maoni.