· Novemba, 2009

Habari kuhusu Sheria kutoka Novemba, 2009

Ufaransa: Tuzo ya Fasihi Yaja na Masharti

  19 Novemba 2009

Mwanzo wa msimu wa Fasihi ya Kifaransa mwaka huu ulishuhudia mwandishi wa riwaya na michezo ya kuigiza mwenye asili ya Kisenegali na Kifaransa Marie N’Diaye akipewa tuzo iliyosuburiwa sana ya Prix Goncourt. Lakini, N’Diaye na familia yake walikwishahamia mjini Berlin miaka miwili iliyopita, hasa kutokana na siasa za rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy. Mwaka jana, jopo la tuzo hii yenye hadhi walizusha hisia kali pale walipomchagua mwandishi wa Kiafghani Atim Rahimi, kwa kitabu chake cha Kifaransa, Syngué Sabour. Je hii itakuwa ni fursa nyingine ya kusherehekea mchanganyiko wa aina mbalimbali katika jamii inayobadilika ya Kifaransa? Au itakuwa ni wasaa utakaoharibiwa na utete wa tukio?

Misri: Haki ya Kijerumani kwa Marwa El Sherbini

Muuaji wa Marwa El-Sherbini, mwanamke wa Kimisri ambaye alichomwa visu mpaka kufa na muhamiaji mwenye asili ya Urusi na Ujerumani, Alex Wiens, ndani ya mahakama huko Ujerumani, amehukumiwa kifungo cha maisha, bila uwezekano wa kuachiwa mapema. Haki hatimaye imetolewa na muuaji anaadhibiwa, wanasema wanablogu wa Misri.

Video: Dunia Yaadhimisha Kuanguka kwa Ukuta wa Berlini

  11 Novemba 2009

Leo ni Kumbukumbu ya 20 ya kuanguka kwa Ukuta wa Berlini, kizingiti madhubuti cha kiusalama ambacho kiliwahi kuligawa jiji la Berlini katika pande mbili za Mashariki na Magharibi huko Ujerumani. Leo tunaonyesha baadhi ya picha za video zinazotoka pande mbalimbali za dunia zinazopandishwa ili kusherehekea siku hii na nini ukuta huo ulimaanisha siyo Ujerumani tu bali duniani kote.

Pakistani: Katika Vita

  4 Novemba 2009

Mohammad Malick anatoa maoni juu ya shambulizi la kigaidi la hivi karibuni kwenye soko la watu wa tabaka chini na la kati huko Peshawar: “limeonyesha kuwa hii ni vita ambyo magaidi wanasimama upande mmoja wa mstari wa damu, na sisi wananchi upande mwingine.”