Habari kuhusu Sheria kutoka Julai, 2010
Brazil: Ukatili Dhidi ya Wanawake Kila Siku
Nchini Brazil, wanawake 10 huuwawa kila siku. Mauaji ya hivi karibuni na anasadikiwa kuwa mzazi wa mtoto wake, mlinda mlango nyota aneyetarajiwa, yamewasha cheche za majadiliano katika uwanja wa blogu kuhusu ukatili dhidi ya wanawake.
Thailand: Vurugu Zinazotokana na Ujumbe Mfupi wa Maneno wa Waziri Mkuu
Wakati Waziri mkuu wa Thailand Abhisit Vejjajiva alipotwaa madaraka mwaka 2008, alituma ujumbe mfupi wa maneno kwa mamilioni ya wateja wa simu za viganjani wa Thailand akiwataka wawe na umoja. Hivi sasa anakabiliwa na makosa ya ufisadi kwa kupokea "zawadi" kutoka mashirika ya mawasiliano. Kadhalika anashutumiwa kwa kuvunja mipaka ya ya faragha za wateja wa simu za viganjani.
Asia ya Kusini Mashariki : Ngono na Udhibiti wa Mtandao
Uratibu wa maudhui katika intaneti unaonekana kana kwamba ni kinyume na demokrasia lakini serikali za Kusini Mashariki mwa Asia zinaweza kuhalalisha kitendo hicho kwa kuzusha haja ya kuwaokoa vijana kutoka kwenye janga la tabia za ngono holela.