· Septemba, 2008

Habari kuhusu Sheria kutoka Septemba, 2008

Sheria inapokwaza haki za binadamu …

  29 Septemba 2008

Mtoto mwenye umri wa shule ya msingi aliyepatikana nje ya ndoa huko Zhuhai, kusini mwa China, hakubaliwi kujiunga na shule, kwa sababu mama yake hawezi kulipa faini kubwa ya kuwa na "mwana haramu", habari hii inasimuliwa na bloga, Han Tao.

Venezuela: Wahindi wa Yukpa, Chavez na Mgogoro wa Ardhi

  6 Septemba 2008

Picha za video zinazotumwa kwenye mtandao wa internet na vyombo vya habari vya kiraia zinaonyesha yale yanayojiri kuhusu mgogoro unaoibuka nchini Venezuela kati ya Wahindi wa jamii ya Yukpa wanaoishi katika milima ya Perijá, wamiliki wa ardhi na Rais Chávez. Mgogoro huu kuhusu mipaka ya ardhi umekuwapo kwa takribani miaka 30, yaani tangu pale vikosi vya jeshi vilipowandoa kwa nguvu wanajamii wenyeji ya Ki-Yukpa na kuwapa ardhi hiyo wamiliki wapya walioanzisha mashamba makubwa ya mifugo, hasa ng'ombe, ambao wameendelea kuitumia ardhi hiyo tangu wakati huo.