Habari kuhusu Kiingereza kutoka Januari, 2010
Misri: wanablogu Watiwa Mbaroni Kufuatia Kutembelea kwao Naha Hammady
Leo Misri iliwatia mbaroni wanablogu 20 waliokuwa wakitembelea eneo la Naga Hammady huko Misri ya Juu ili kutoa heshima zao kwa watu waliouwawa katika shambulio la kidini mnano January 7 mwaka huu. Watu 7 waliuwawa kwa risasi huku wengine wengi wakijeruhiwa pale mwuaji alipowamiminia risasi Wakristo wa Madhehebu ya Kikopti waliokuwa wakitoka kanisani mara baada ya Misa ya Krismas (Wakopti husherehekea Krismas kila tarehe 7 Januari). Uamuzi wa kutembelea eneo hilo uliofanywa na wanablogu hao ulikuwa ni kwa lengo la kuungana dhidi ya uhasama wa kidini.
Haiti: Uenezaji Habari na Taarifa
Sisi tulio nje ya Haiti tunaweza tu kujenga picha kichwani kuhusu hali halisi ya maisha ya kila siku yalivyo huko baada ya tetemeko baya la ardhi - lakini katikati ya juhudi za kuwatafuta wapendwa ndugu, juhudi za kuwahudumia waliojeruhiwa na jukumu zito na gumu la kuwafikishia msaada wa kiutu wale wanaouhitaji zaidi - wanablogu walio huko Port-au-Prince na maeneo ya jirani wanawasiliana na ulimwengu wa nje, ambao nao unahangaika kutaka kupata taarifa kutoka kwa wale waliokuwa katika eneo lenyewe kabisa la janga.
Haiti: Twita Kutoka Eneo La Tukio
Wakati habari za tetemeko la ardhi huko Haiti zikitoa mwangwi duniani kote, wakazi majasiri, wanahabari wan je, na wafanyakazi wa misaada wanaandika jumbe za twita kutokea katika eneo lililoathirika. Baadhi yao wanafanya kazi ya kukusanya misaada na fedha, wakati wengine wanajaribu tu kuionyesha dunia mambo yanavyooendelea nchini Haiti.
Haiti: Madhira ya Tetemeko la Ardhi
Mpaka sasa taarifa za majeruhi wanaotokana na tetemeko la ardhi lililoikumba Haiti zimejikita kwenye takwimu za kutisha, lakini ni majina machache tu ndiyo yameambatanishwa kwenye namba hizo. Katika makala hii tunapata simulizi za wale walionusurika kutoka kwenye janga hili la asili kama wanavyozirusha kwenye mtandao.
Baada Ya Tetemeko la Ardhi, Jumbe za Twita Kutoka kwa Walioshuhudia
Kutokana na janga la tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 7.0 ambalo limekikumba kisiwa cha Haiti jioni ya leo (Januari 12), “Haiti” ni mada kuu hivi sasa kwenye huduma ya Twita. Miongoni mwa lundo la jumbe zinazotumwa tena na tena za taarifa za habari kutoka za vyombo vya habari vikubwa na jumbe nyingine za twita zinazotuma sala au dua pamoja na salamu za heri kwa kisiwa hiki cha Karibea, pia kumekuwepo taarifa za mashahidi waliopo kwenye tukio kama vile mwanamuziki na mwendesha hoteli Richard Morse, ambaye anatwiti kwa jina la @RAMHaiti.
China: Kwa Heri Google
Kufuatia tangazo la Google leo kuwa ikiwa serikali ya China haitaruhusu tawi lake la China kusitisha uzuiaji wa matokeo ya kutafuta tawi la Google nchini China litafungwa, wanamtandao walitembea mpaka kwenye ofisi za Google mjini Beijing ili kuweka maua. HABARI MPYA: picha zaidi hapa, uwekaji rasmi wa maua (ya rambirambi)...
Afrika: Matangazo ya “AdWords” Katika Afrika
Miquel anajadili matangazo ya Google AdWords katika Afrika: “Wakati ingelikuwa ni njia nzuri sana kwa wanablogu wa Kiafrika kupata pesa kidogo ili kulipia gharama za intaneti, Google haitoi chaguo la malipo kwa nchi yoyote ya Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara.”
Misri: Mauaji ya Kinyama ya Naga Hammady
Wanablogu wa Misri wanaelezea kustuka kwao na hasira kwa kuuwawa kwa Wakristu wa dhehebu la Koptiki wakati wa mkesha wa sikukuu yao ya krismasi huko Naga hammady, katika Misri ya Juu. Mhalifu asiyejulikana alipiga risasi hovyo hovyo kwenye umati watu baada ya waumini kumaliza maombi na wakiwa wanaelekea majumbani kwao.
Angola: Kombe La Mataifa ya Afrika Moja Kwa Moja Kwenye Mtandao
Pata habari za Kombe la Mataifa ya Afrika yanayofanyika nchini Angola moja kwa moja: “Kwa wale ambao wangependa kuangalia Kombe la Mataifa ya Afrika 2010 kwenye mtandao, kutakuwa na tovuti za michezo zinazotoa mtiririko wa mapambano ya mpira moja kwa moja mtandaoni, bure.”
Thailand: “Tumechoshwa na Wizara ya Utamaduni”
Ukurasa wa wapenzi wa Facebook umezinduliwa na raia wa mtandaoni wanaokosa njia na sera za Wizara ya Utamaduni ya Thailand. Wizara hiyo imekuwa ikidhibiti sana uhamasishaji na usimamizi wa utamaduni wa asili wa Ki-Thai katika tovuti za vyombo vya habari vya kizamani na hata vile vya kisasa.