Habari kuhusu Pakistan

PICHA: Maandamano ya Pamoja ya Watu wa Shia Nchini kote Pakistan Yamalizika Kwa Amani.

  12 Februari 2013

Baada ya milipuko ya mabomu huko Quetta kuua zaidi ya watu 100, maanadamano ya watu wa jamii ya Hazara ya Shia yalisambaa kama moto katika maeneo mbalimbali ya Pakistani. Watu kutoka katika makundi makuu ya dini na makabila mbalimbali waliungana kwa pamoja na watu wa Hazara wakiimba kwa kurudiarudia#Sisi sote ni watu wa Hazara. Maandamano ya kuishinikiza serikali kusikiliza madai yao yalianzishwa katika zaidi ya majiji 100 na miji.

Mwanaharakati wa Pakistani Khudi Ali Auawa Katika Mlipuko wa Bomu

  14 Januari 2013

Mnamo Januari 10, 2013 katika jiji la Quetta lililopo Kaskazini Mashariki mwa nchi ya Pakistani, watu 82 walipoteza maisha kwenye milipuko ya mabomu yaliyolenga eneo ambalo kimsingi lenye idadi kubwa ya Waislamu wa Shia jamii ya Hazara. Irfan Khudi Ali, mwanaharakati mashuhuri wa haki za binadamu ambaye bila kuchoka aliweka wazi uonevu wa kikabila unaofanywa kwa waShia wa Hazara nchini Pakistan, alifariki katika shambulio lililofuata. Kifo chake kimechochea watu kumpa heshima kwa juhudi zake kwa kuanzisha tena maandamano kupinga mauaji ya watu wa Shia nchini Pakistani.

Maelfu Watia Saini Pendekezo la Zawadi ya Nobel na Kusherehekea Siku ya Malala

  12 Novemba 2012

Mwanaharakati wa elimu mwenye umri wa miaka 15 -- Malala Yousufzai -- aliyepigwa risasi mnamo tarehe 9 Oktoba 2012 na wanamgambo wa TTP, anaendelea kupata nafuu japo polepole. Mnamo tarehe 10 Novemba, watu kote ulimwenguni walimpongeza Malala kama kielelezo kwa ajili ya wasichana wapatao milioni 32 ambao hawapati fursa ya kwenda shulen.

Pakistani: Msichana wa Kikristo wa Miaka 11 Awekwa Kizuizini kwa Kukashifu Dini.

  16 Septemba 2012

Rimsha Masih msichana Mkristo mwenye umri wa miaka 11 ametuhumiwa kwa makosa ya kukashifu na ameshikiliwa kwa siku kumi na nne katika gereza za watoto huko Rawalpindi, nchini Pakistani. Anashitakiwa kwa kuchoma kurasa za kitabu cha Noorani Qaida, kinachotumika kwa wanafunzi wa lugha ya kiarabu, na kuziweka katika mfuko wa 'rambo'.

Pakistani: Buriani Mehdi Hassan; Mfano wa kuigwa wa Ghazal.

  23 Juni 2012

Mehdi Hassan Khan ambaye maarufu alijulikana kama ‘Mfalme wa Ghazal’alifariki dunia Jumatano tarehe 13, Juni, 2012 baada ya kuugua kwa muda mrefu, katika hospitali jijini Karachi nchini Pakistan. wananchi wa Mtandaoni wanattoa salamu zao za mwisho.

Tunisia: Picha ‘Zilizochakachuliwa’ ni Dalili ya Hali Halisi katika Vyombo vya Habari vya Kitaifa

Utumiaji vyombo vya habari vya kitaifa nchini Tunisia kama chombo vya kupigia propaganda ni jambo ambalo limeripotiwa vya kutosha. Ushahidi wa hivi karibuni kabisa wa utumiaji mbaya wa vyombo vya habari umewekwa bayana na wanablogu wa nchi hiyo mnamo tarehe 20 Agosti baada ya magazeti ya Le Temps na Assabah kuchapisha ripoti kuhusu taasisi ya hisani ya Zeitouna kutuma msaada wa kibinadamu wa chakula kwa waathirika wa mafuriko nchini Pakistani.

India, Pakistani: Hekaheka za Sania-Shoaib Zaendelea

  14 Aprili 2010

Utata wa harusi ya Shoaib Malik na Sania Mirza unaendelea huku vyombo vya habari vikichochea hekaheka na mamilioni ya watu nchini India na Pakistani wanaendelea kuzama katika habari hiyo. Wakati wapenzi hao wanajiandaa na harusi na kuvishinda vikwazo, sehemu nyingine mashambulizi yanaendelea.

Kuchapisha Bloguni kuhusu Utamaduni na Ndoa za Watu wa Asili Tofauti

  6 Januari 2010

Idadi kadhaa ya familia zinazoundwa na watu wa rangi na dini tofauti wanasimulia kuhusu uzoefu wa maisha yao katika familia zao kupitia ulimwengu wa blogu. Majaribu na mahangaiko ya wanandoa wenye asili tofauti yanaonyesha, kama kioo, jinsi sisi, kama watu tuliostaarabika, tulivyotoka mbali na hasa katika kupokea na kuheshimu tofauti zetu.