Habari kuhusu Pakistan
GVFace: Kuvunja Ukimya wa Pakistani Kuhusu Mapigano Yanayoendelea Jimbo la Balochistani

Mijadala wa wazi kuhusu vita vinavyoendelea kwenye jimbo la Balochistani ni nadra. Wanaotetea umoja wa nchi hiyo wanadhani kimya kuhusu jimbo Balochistan ni wajibu wao wa kizalendo, wengine wakijizuia kwa hofu ya nguvu ya kijeshi ya Pakistani.
Kikundi cha Kitalibani Chasema Shambulio la Uwanja wa Ndege wa Karachi Lililoua Watu 24 Lilikuwa ‘Kisasi’
Ingawa wanamgambo wanaosemekana kuingia kwenye sehemu ya zamani ya kupumzikia abiria ambayo ilikuwa imetengwa kwa ajili ya watu maarufu na ndege za Hajj, bado sehemu zote hizo zina njia moja tu ya kutua na kupaa ndege na magaidi wameidhibiti.
Baada ya Waziri wa India Kusema ‘Wakati Mwingine Ubakaji Unakubalika’, Kampeni ya #MenAgainstRape Yavuma Nchini Pakistani
Mamia wa vijana wa kiume kutoka Pakistani wameingia mtandaoni wakifanya kampeni ya kupinga ubakaji
Mazungumzo ya GV: “Mtandao wa Twita” wa Siri wa Kimarekani Nchini Cuba

Mpango wa siri wa Marekani wa kubadili utawala nchini Cuba wenye huduma ya ujumbe inayofanana na Twita iitwayo ZunZuneo sasa unaangaliwa kwa mashaka baada ya kuwepo kwa taarifa kuwa maelfu...
Pakistan, Usiingilie Vita vya Ndani ya Syria
Siku moja baada ya dondoo ndogo ya habari yenye kichwa cha habari, “Saudi Arabia ‘inatafuta uungwaji mkono kwa waasi wa” ilipoonekana kwenye magazeti ya Pakistani, mwanablogu wa siasa Ahsan Butt...
Sababu 10 Kwa nini Siafiki Shariah Nchini Pakistan
Mmoja wa msemaji wa Taliban alijitoa kwenye majadiliano ya hivi karibuni na serikali ya Pakistan na kudai kuwa ajenda ni pamoja na kuanzishwa kwa sharia kali. Mwanablogu wa Pakistan na...
Nani ni Muislamu Halisi? -Hatari ya Madhehebu Madogo ya Waislamu Pakistan
Raza Habib Raja wa Pak Tea House ana maoni haya: ‘Kosa’ kubwa nchini Pakistani ni kuwa kile ninachokiita, Muislamu asiye Muislamu. Kwa hiyo hata ukiwa Ahmedi, Shiite, na hata muumini...
Kuwasaidia Waathirika wa Tetemeko la Balochistan
Zaidi ya watu 300,000 wameathirika kufuatia tetemeko la hivi karibuni katika wilaya sita za Jimbo la Balochistan nchini Pakistan. Kashif Aziz wa mtandao wa Chowrangi anatoa habari za namna ya...
Mama na Watoto Wake Wauawa kwa Kucheza kwenye Mvua
Mama na watoto wake wawili wa kike waliuawa kwa kufyatuliwa risasi mara baada ya watu watano waliokuwa wamefunika nyuso zao kuvamia nyumba alimokuwa akiishi mama huyu na watoto wake katika mji mdogo wa Chilas nchini Pakistan, tukio linalosadikiwa kuwa ni la mauaji ya kulinda heshima. Video iliyorekodiwa kwa simu inayowaonesha wasichana hao wakicheza kwenye mvua imekuwa ikisambaa kiholela na ambayo imeonekana kama ni kashfa na hivyo kuharibu heshima ya familia.
Pakistan: Imran Khan Aanguka na Kuumia Akiwa Kwenye Jukwaa la Kampeni
Aliyekuwa mchezaji maarufu wa kriketi na kisha kuamua kuwa mwanasiasa, ambaye kampeni yake ina tumaini kubwa la kuleta "Pakistan Mpya" aliyeweza kushawishi idadi kubwa ya vijana pamoja na wapiga kura wanaotokea mijini katika mikutano yake, alivunjika vifupa vitatu vya uti wa mgongo pamoja na mbavu baada ya kuanguka kutoka kwenye winchi iliyokuwa katika kimo cha futi 15 mda mfupi kabla ya kuhutubia. tukio hili limeonekana kuliunganisha tena taifa hili lililojigawa kwa visasi vinavyotokana na uchaguzi utakaofanyika mapema wiki hii.