Habari kuhusu Kiingereza kutoka Februari, 2009
Malawi: Homa Ya Uchaguzi na Kuelea Teknolojia ya Kidijitali
Juma lililopita lilikuwa lenye moto wa kisiasa kwa Wamalawi wengi kwani wameshuhudia wagombea wa viti vya urais na ubunge wakiwasilisha maombi yao kwenye Tume ya Uchaguzi kuelekea Uchaguzi utakaofanyika terehe 19 Mei. Hadi kufikia mwisho wa zoezi hilo wagombea wapatao 10 waliwasilisha maombi yao ya kugombea urais na mamia wengine kwa ajili ya kugombea viti 193 vya bunge.
Karibeani Ya Kifaransa: Tamasha la Kanivali 2009 Lazinduliwa
Kanavali ni utamaduni, sehemu ya uhai wa kila Muhindi wa Magharibi bila kuwaacha wale wa Karibeani ya Kifaransa. Ufuatao ni muhtasari wa blogu kutoka Martiniki, Guyana ya Kifaransa, Haiti na Guadalupe, ambao unaelezea mambo yanavyokuwa kwenye Kanivali.
Kampuchea: Vikwazo Vya Intaneti Vyalenga Wasanii
Wizara ya Masuala ya Wanawake nchini Kampuchea imetishia kuizuia tovuti yenye michoro ya wacheza ngoma ya Apsara walio vifua wazi pamoja na mwanajeshi wa Khmer Rouge. Uchujwaji wa habari wa namna hii unawalenga wasanii wanaotambulika zaidi kwa uwepo wao katika mtandao wa intaneti.
Bahrain: Mabloga Waungana Kupinga Uamuzi wa Kufungwa Kwa Tovuti
Wanablogu wa Bahrain wameujia juu uamuzi wa Waziri wa Habari wa nchi hiyo wa kuzuia upatikanaji wa tovuti mbalimbali, kadhalika kuzuia matumizi ya tovuti vivuli [proxy sites] zinazoruhusu watumiaji kuperuzi tovuti nyingine zilizozuiwa na zana za kuchuja habari. Ayesha Saldanha anaangalia maoni kutoka Bahrain.
Mashariki ya Kati: Vikwazo kama Silaha ya Kisiasa
Watu wengi wa Mashariki ya Kati wamesusia bidhaa za Israeli na Marekani kama jibu la mashambulizi ya Israeli huko Gaza. Tarek Amr anapitia yale wanablogu wanayosema kuhusu suala hili.