Habari kuhusu Brazil
Togo: Muhubiri Asafirisha Kilo 4.2 za Madawa ya Kulevya Yaliyofichwa kwenye Pipi ‘k Build Church
Muhubiri wa Injili raia wa Togo, Woegna Yao Koufoualesse alikamatwa katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Accra akiwa na kiasi cha kilo 4.2 za madawa ya kulevya aina ya Cocaine akiwa kwenye safarini kutokea Sao Paulo, chapisho la Afrique Infos linaripoti [fr]. Madawa hayo yalikuwa yamefichwa ndani ya peremende za...
Brazili: Jarida Lawapa Nafasi Wasio na Makazi
Jarida la Ocas linalosambazwa katika mitaa ya mjini São Paulo pamoja na Rio de Janeiro tangu 2002, ni jarida ambalo husheheni habari ambazo hulitofautisha na vyombo vikuu vya habari nchini Brazil. Na linakwenda zaidi ya hapo. Aidha huwapa mwanzo mpya na fursa za kazi watu ambao hawana makazi na ambao wamo katika hatari ya kuangamia kijamii.
Dondoo za Video: Utetezi wa haki za binadamu
Kuna masimulizi kusisimua katika siku za hivi karibuni kwenye tovuti ya Global Voices Video za Utetezi ikiwa ni pamoja na haki za wananchi wenyeji na habari za hivi karibuni kutoka Amerika ya Kusini, Mashariki ya Mbali, Ulaya Magharibi na Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara zilizochaguliwa na Juliana Rincón Parra.
Brazil: Leo Rais, Kesho Mwanablogu
Rais wa Brazil anayeondoka madarakani Luis Inácio Lula da Silva (Lula) alihojiwa na wanablogu wapenda maendeleo (au wenye mlengo wa kati kuelekea kushoto) kwa mara ya kwanza wiki hii, tukio ambalo limechukuliwa na wengi kama hatua muhimu katika msukumo uliopo unaotaka mfumo wa habari wa kidemokrasia zaidi nchini Brazil.
Brazil: Uchaguzi Safi kwa Mtindo wa “Jifanyie Mwenyewe”
Chini ya mwezi mmoja ujao kutakuwa na uchaguzi nchini Brazil na mradi wa Eleitor 2010 tayari umekwisha kuwa na nguvu za kubadili mchakato huo: ni mradi wa “vyanzo vya habari vya kiraia” ambao una lengo la kuratibu taarifa za raia zinazoripoti ukiukwaji wa mchakato wa uchaguzi nchini Brazil. Kwa kupitia jukwaa hilo, kuna simulisi kadhaa za kuburudisha ambazo zimeshaanza kujitokeza.
Brazil: Ukatili Dhidi ya Wanawake Kila Siku
Nchini Brazil, wanawake 10 huuwawa kila siku. Mauaji ya hivi karibuni na anasadikiwa kuwa mzazi wa mtoto wake, mlinda mlango nyota aneyetarajiwa, yamewasha cheche za majadiliano katika uwanja wa blogu kuhusu ukatili dhidi ya wanawake.
Brazili: Ulimwengu wa blogu waunga mkono sheria ya kuzuia ufisadi
Muswada wa sheria kwa ajili ya kuwazuia wanasiasa ambao wamewahi kutenda makosa makubwa ya jinai ili wasigombee nafasi za kuchaguliwa umeanza kuzua kizaazaa nchini Brazili huku karibu watu milioni 2 wakitia saini zao kama ishara ya kuunga mkono.
Siku ya Ada Lovelace: Kuwapongeza Wanawake Wanajishughulisha Kupigania Teknolojia na Uwazi Ulimwenguni
Katika kusherehekea Siku ya Ada Lovelace tunawaletea makala fupifupi kuhusu wanawake kadhaa walio sehemu mbalimbali duniani ambao hutumia teknolojia ili kuzifanya serikali ziwe wazi na zinazowajibika zaidi.
Brazil: Wito wa Kugomea Gazeti Linaloongoza Nchini
Wanablogu wa Brazili wamekuwa wakihamasisha mgomo dhidi ya kile walichokiita Coupist Press Party, yaani Sherehe ya Chombo cha Habari ya Kutaka Kupindua Serikali, kwa hiyo wamekuwa wakiwataka watu kuacha kununua, kusoma au kutoa maoni na badala yake kufuta usajili wao kutoka kwenye gazeti la Folha de São Paulo na tovuti yake.
Brazil: Je, Milango ya Benki Hubaini vyuma au Rangi za Watu?
Benki nyingi nchini Brazil zinatumia milango inayozunguka yenye vifaa vya kubaini vyuma. Je, milango hiyo inatumika kama kisingizio cha kubagua watu? Video ya uandishi wa kiraia inaonyesha moja ya matukio hayo.