Habari kuhusu Paraguai

Wikipedia kwa Lugha ya Ki-Guarani

Mwaka huu, Wikipedia katika lugha ya Kihispaniola ilifikia makala milioni moja na kutolewa kwa mwongozo msingi wa mtumiaji katika lugha ya ki-Guarani. Wazo ni kufufua jamii ya wanaozungumza kiguarani katika...

2 Novemba 2013

Paraguai: Kutoka Kutumikishwa Hadi Kuwa Kiongozi Mzawa.

Sauti Chipukizi

Kutana na Margarita Mbywangi, ambaye katika umri wa miaka mitano, alichukuliwa kutoka kwa wazazi wake na kuuzwa mara kadhaa na kulazimishwa kufanya kazi za nyumbani. Tangu wakati huo amekuwa kiongozi muhimu wa kabila la Aché na hata kuwa Waziri katika nchi yake. Mbywangi sasa anasimulia maisha yake binafsi kupitia Mradi wa Rising Voices.

21 Julai 2012

Paraguay: Wenyeji Wanyunyiziwa Dawa za Kuua Wadudu kwa Ndege

Huko Mashariki mwa Paraguay, jumla ya watu 217 wa jumuiya ya wenyeji ya Ava Guaraní walianza kusumbuliwa wakionyesha dalili mbalimbali za kiafya zinazoaminika zilisababishwa na unyunyiziaji wa makusudi wa dawa za kuua wadudu hasa baada ya wao kuwa wamegoma kuhama kutoka katika ardhi waliyoirithi kutoka kwa mababu zao.

17 Novemba 2009

Paraguai: Rais Lugo Akiri Kuzaa Mtoto Wakati Bado Akiwa Askofu

Hivi karibuni Rais wa Paraguai Fernando Lugo alikiri kuwa alizaa mtoto wakati alipokuwa askofu wa kanisa la Katoliki la Roma. Habari hii imesababisha utata kati ya wanasiasa, vyombo vya habari, na wanablogu ambao wanaandika kuhusu kusikitishwa kwao na kiongozi huyo, na kadhalika jinsi ambavyo kuna matatizo mengine makubwa zaidi yanayotisha ambayo yanapaswa kutiliwa mkazo ikilinganishwa na vitendo vinavyofanywa na wanasiasa wengine.

19 Aprili 2009

Paraguai: Wahamiaji Wasimulia Visa Vyao

Ni jambo la kawaida katika Marekani ya Latini kwa wahamiaji kuondoka na kwenda kwenye malisho ya kijani zaidi kwenye nchi jirani au nchi za mbali. Hakuna tofauti kwa Waparaguai, ambao huwaacha nyuma marafiki zao na familia ili kufuata fursa nyingine. Simulizi kadhaa za namna hiyo zinasimuliwa kwenye blogu inayoitwa Paraguayos (sisi ni Waparaguai), ambayo inawaalika wahamiaji walioko duniani kote kuwasilisha simulizi zinazohusu uzoefu wao.

22 Februari 2009

Paraguai: Rais Lugo Kutopokea Mshahara

Utawala wa Rais Ferdinand Lugo umeanza na tangazo kuwa hatapokea mshahara wake wa mwezi. "Sihitaji mshahara huo, ambao unapaswa kumilikiwa na masikini," alisema Lugo. Mabloga nchini humo wanatofautiana mitazamo, wakati mmoja anausifu uamuzi huo, mwingine anajiuliza ni vipi Rais lugo atajilipia gharama binafsi za maisha.

12 Septemba 2008

Paraguai: Kuapishwa Kwa Lugo Kwenye Flickr

Rais wa paraguai alianza kutumia Flickr mnamo januari 2008 kama njia ya kuorodhesha nyendo zake wakati wa kampeni. Baada ya kuapishwa kama rais wa nchi siku ya tarehe 15 Agosti, anaendelea kutumia chombo hiki cha uandishi wa kijamii. Karibia picha 2,500 baadaye na zote chini ya haki miliki huria, Lugo anategemea kuwajumuisha WaParaguai nyumbani na ughaibuni katika urais wake.

12 Septemba 2008