Habari Kuu kuhusu Chile
Habari kuhusu Chile
Podikasti ya Chile Yafanya Nyota za Anga Zionekane na Kila Mtu
"Shauku yangu kuu ni kwetu sote kumgundua mtoto aishiye ndani yetu na kushangaa namna ulimwengu tunaoishi ulivyo wa ajabu."
Kwenye Mtandao wa YouTube, Vichesho vya Namna Sikukuu za Krimas Zinavyoadhimishwa Amerika Kusini
Ucheshi: Moja ya alama muhimu ya sikukuu za Krismas barani Amerika ya Kusini.
Wanafunzi Waandamana Nchini Chile Kudai Mageuzi ya Kielimu
Katika maeneo kadhaa nchini Chile, maandamano ya wanafunzi kudai elimu ya bure na kushirikishwa kwenye mabadiliko yanayoendelea nchini humo yalifanywa Mei 8, 2014. Hata hivyo, yalikabiliwa na bughudha za hapa na pale.
Tetemeko Kubwa Lizitikisa Chile na Peru
Watumiaji wa mtandao wa twita wameripoti kuwa huduma za simu za mkononi hazipatikani na umeme umekatika kwenye maeneo kadhaa ya Peru.
Tetemeko Kubwa Laitikisa Chile Kaskazini, Lafuatiwa na Tahadhari ya Tsunami
Tetemeko kubwa lenye vipimo vya 8.2 limeikumba Chile kaskazini saa 2:46 na kusababisha tahadhari ya tsunami nchini kote.
VIDEO: Kuelekea Mfumo wa Haki na Jumuishi Nchini Chile
Katika video hiyo hapo juu iliyowekwa na Mfuko wa Jamii Wazi , Giorgio Jackson, kiongozi wa zamani wa wanafunzi na mbunge mpya kabisa nchini Chile, anajadili mfumo wa elimu nchini mwake na maanaa hasa ya kuwa “jamii wazi”. Trine Petersen anaandika: Mfumo wa haki na jumuishi unaoifanya elimu ipatikane kwa...
Chile: Tetemeko la Ardhi Lafichua Ukosefu wa usawa Katika Jamii
Ukiukwaji sheria kulikojitokeza baada ya tetemeko la ardhi la Februari 27 nchini Chile kumezua mjadala wa kitaifa kuhusu kutokuwepo kwa usawa wa kijamii na kiuchumi nchini.
Video: Tetemeko la Ardhi Chile Kwa Kupitia Macho ya Raia
Wakati siku inakaribia kuisha, video zaidi za tetemeko la ukubwa wa 8.8 ambalo liliikumba Chile majira ya saa 9.30 usiku zinajitokeza. Tetemeko hilo, ambalo halikuathiri maeneo ya bara pekee kwa njia ya kusogea sogea kwa ardhi, kadhalika lilisababisha mawimbi ya tsunami mabyo yalizua tahadhari katika eneo zima la Pasifiki huku mataifa mbalimbali yakijiandaa kwa mawimbi hayo pindi yatakapofika kwenye fukwe zao.
Chile: Tetemeko Kubwa la Ardhi lenye Ukubwa wa 8.8 Laikumba Chile
Saa 9:34 usiku kwa saa za Chile, tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 8.8 liliukumba mwambao wa eneo la Maule nchini Chile. Tetemeko hilo liliutetemesha mji mkuu wa Santiago uliopo Kilomita 325 kutoka katika kiini cha tetemeko hilo. Uharibifu mkubwa umeripotiwa nchin nzima, na idadi ya waliofariki inazidi kwenda juu.
Amerika ya Kati: Kasi Kubwa ya Ueneaji wa Jangwa
Ueneaji wa jangwa unasambaa kimyakimya lakini kwa kasi kubwa mahali pengi duniani na Amerika ya Kati haijaweza kukwepa hali hii iliyo na athari mbaya za kutisha. Wakati ambapo majangwa ni maumbo ya asili, ueneaji wa jangwa ni mchakato wa kuharibika kwa nyanda za ardhi kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na uharibifu unaofanywa na binadamu.