Habari kuhusu Kiingereza kutoka Februari, 2014
Sababu 10 Kwa nini Siafiki Shariah Nchini Pakistan
Mmoja wa msemaji wa Taliban alijitoa kwenye majadiliano ya hivi karibuni na serikali ya Pakistan na kudai kuwa ajenda ni pamoja na kuanzishwa kwa sharia kali. Mwanablogu wa Pakistan na Mwandishi wa Habari Beena Sarwar alipinga wazo hilo kupitia tamko aliloliweka katika mtandao wa Facebook lenye kichwa cha habari ‘sababu...
Sinagogi Pekee Lililobaki Myanmar
Lilijengwa miaka 120 iliyopita, Sinagogi la Musmeah Yeshua lililoko eneo la Yangon ni Sinagogi pekee la wayahudi lililoyobaki katika eneo linaloongozwa na waumini wa dini ya Kibudha waishio nchini Myanmar. Mbali na kuwa kivutio cha utalii, pia limetajwa kama jengo la urithi la mambo ya kale katika mji huo.
Rais Yanukovych wa Ukraine ang'olewa madarakani
Baada ya maandamano, vurugu na upinzani dhidi ya serikali uliosababisha vifo vya watu wapatao 100, Bunge la Ukraine hatimaye limepiga kura ya kumwondoa Rais Viktor Yanukovych kama hatua ya kujibu shinikizo la waandamanaji. Tayari Rais Yanukovych amenukuliwa akisema hana mpango wa kutoroka nchi. Soma zaidi kupitia kiungo hiki [en]
Upasuaji wa Kwanza wa Moyo Kongo Brazzaville
Mtandao wa kimataifa wa Afya La Chaîne de l’Espoir (Maana yake Kiungo cha Matumaini) unaripoti kuwa watoto saba wa ki-Kongo waliokuwa na hali mbaya wamenufaika na upasuaji wa moyo [fr] uliofanyika Februari 14 mjini Brazzaville, Kongo. Kwa msaada wa Msaidizi wa Kongo Shirika lenyewe, Prince Béni na Maya, wote wakisumbuliwa na...
Vyombo Vikuu vya Habari Vyaihujumu Facebook
Mwanablogu wa Teknolojia Amitha Amarasinghe anadai kwamba mtandao wa Facebook unapewa taswira hasi na vyombo vikuu vya habari nchini Sri Lanka kwa vichwa vya habari kama “Mwanafunzi ajiua shauri ya picha iliyowekwa Facebook”, “Mapenzi ya Facebook yaishia na kifo” na kadhalika. Ghafla tu, kuna mwongezeko mkubwa wa maudhui yanayotoa taswira...
Wamalagasi Wajadili Kivazi na Maoni ya Mlimbwende wa Kigeni Kuhusu Madagaska
Picha ya Tangazo la Kivazi cha Kuogolea 2014 iliyopigwa eneo la (kisiwa cha) Nosy Iranja, Madagaska: Nosy Iranja ni kisiwa kinachofahamika kama Turtle kwa sababu viumbe waitwao Hawksbill Turtles walikuja ufukweni kutaga mayai yao. Kisiwa hicho pia kinafahamika kwa mchanga wa pekee unaounganisha visiwa hivyo viwili. Mlimbende mashuhuri wa ki-Rusi...
Tafakuri kwenye Mkutano Mkubwa Zaidi wa Blogu Nchini India
#WIN14, mkutano mkubwa zaidi na tuzo zinazoongoza nchini India, unaoandaliwa na BlogAdda, ulifanyika Februari 89, 2014. Mwanablogu Dk. Roshan Radhakrishnan, aliyeshinda tuzo ya blogu bora ya uandishi wa ubunifu nchini India, anatoa maoni na picha zake.
Pongezi kwa Waziri Mkuu Mpya wa Nepal
Bunge la Nepal limemchagua Bw. Sushil Koirala (75), rais wa chama cha Nepali Congress, kuwa Waziri Mkuu wa Nepal. Mwanablogu wa NNepali aishiye ughaibuni Indra anampongeza Waziri Mkuu mpya na anafikiri kwamba “zawadi aliyonayo Bw. Koirala kwa kuwawezesha wengine kwa unyenyekevu na ukweli haitaondoka wa haraka”.
Mwandishi Mwandamizi wa Kichina Akosolewa kwa Kujifungulia Marekani
"...anachotaka tu ni mwanae awe na mtindo wa kawaida wa maisha, kitu ambacho hakina uhusiano na uzalendo. Labda, hili ndilo tatizo ambalo serikali yapaswa kulitafakari..."
Majadiliano ya GV: Maandamano ya Venezuela
Maandamano ya Venezuela yanahusu nini? Vyombo vya habari za kiraia vina wajibu upi? Tunazungumza na mwandishi wa Global Voices Marianne Díaz kuhusu hali ya mambo inavyoendelea nchini humo hivi sasa.