makala mpya zaidi zilizoandikwa na j nambiza tungaraza kutoka Novemba, 2009
Naijeria: Ken Saro-Wiwa Akumbukwa
Chidi Opara anamkumbuka Ken Saro-Wiwa, Mwandishi wa Kinaijeria, mwanaharakati wa mazingira na haki za walio wachache ambaye aliuwawa na watawala wa kijeshi wa Naijeria tarehe 10 Novemba, 1995.
Kenya: Mwai Kibaki na Odinga Budi Washirikiane na ICC
Ubia wa Kuleta Mabadiliko umetoa tamko linalowataka mwai kibaki na raila odinga kushirikiana na mahakama ya kimataifa ya Jinai na kuhakikisha muswada wa Tume Maalum unapitishwa nchini kenya na kurasimishwa kama sheria ndani ya wiki mbili.
Vijana wa Kiyahudi na Kipalestina Watumia Video Kuuelewa Mgogoro
Mashirika mawili tofauti nchini Israel na katika Majimbo ya Palestina yanatumia zana za video ili kuwasaidia vijana wa Kiarabu na Kiyahudi kuuelewa mgogoro na kujenga daraja kati yao.
Nepal: Mapinduzi Ya Gesi Inayotokana na Samadi
Nchini Nepal karibu asilimia 87 ya kaya zinategemea kuni kama chanzo cha nishati. Hata hivyo, vituo vya kuzalisha gesi inayotokana na samadi vinajitokeza kwa idadi kubwa nchini Nepal na kuanzisha mapinduzi ya kijani.
Cuba: Ukweli wa Sanchez Kutiwa Mbaroni Waibuka
Kukamatwa, kupigwa na kuachiwa huru kulikofuata kwa wanablogu Yoaní Sánchez, Claudia Cadelo na Orlando Luis Pardo kulikofanywa na majeshi ya usalama ya Cuba tarehe 6 Novemba, kunapata matangazo mengi katika vyombo vikubwa vya habari na katika ulimwwengu wa blogu pamoja na ule wa Twita. Yoani ameandika (es) kuhusu tukio hilo...
Yoani Sanchez Pamoja na Wanablogu Wengine wa Cuba Wakamatwa na Kupigwa
Jioni ya tarehe 6 Novemba, blogu ya Babalú iliweka kiungo kuelekea makala iliyoandikwa na Penultimos Dias (es) ilitoa taarifa kuwa baadhi ya wanablogu mashuhuri wa Cuba, wakiwemo Yoaní Sánchez na mchangiaji wa Global Voices Claudia Cadelo, walitiwa mbaroni na majeshi ya usalama. Habari mpya kutoka kwa Penultimos Días zinataarifu kuwa...
Ghana: Vionjo Sehemu ya Kwanza
Sehemu ya kwanza ya vionjo vya Ghana iliyotayarishwa na Gayle: Nchini Ghana, kila kanda ina kitu cha kutoa. Utamaduni, historia, pwani, wanyama na mimea, unaweza ukavivinjari nchini kote, kutokea kwenye mitisitu ya kitropiki kule kusini mpaka mbuga za savana za kaskazini. kama ni mpenzi wa pwani au historia, utaburudika na...
Tunisia: Mwanablogu Fatma Arabicca Awekwa Kizuizini
Mwanablogu wa Kitunisia Fatma Riahi ambaye hublogu kama Fatma Arabicca, ameshtakiwa kwa udhalilishaji katika blogu yake na hivi sasa amewekwa kizuizini.Kundi limeundwa kwenye Facebook kumuunga mkono mwanablogu huyu mwenye umri wa miaka 34, ambaye pia anatuhumiwa kublogu kwenye Debat Tunise (Mdahalo wa Tunisia).
Tamasha la Blogu Indonesia
Tulitembelea tamasha la blogu la Indonesia au PestaBlogger 2009. Hii nim ara ya tatu kwa tukio hili la mwaka kufanyika. Tukio hili lilishuhudia wanablogu kutoka kila sehemu ya Kisiwa hiki ambacho pia ni Taifa wakimiminika mjini Jakarta ili kusherehekea, kujadili na kujumuika.
Misri: Mwanablogu wa Kiume Aagizia Bikra ya Bandia
Mengi yalisemwa na kuandikwa juu ya zana ya kutengeneza bikra ya bandia - mpaka mwanablogu Mmisri wa kiume Mohamed Al Rahhal akanunua moja. Marwa Rakha anatuletea habari hiyo.