makala mpya zaidi zilizoandikwa na j nambiza tungaraza kutoka Novemba, 2009
Misri: Haki ya Kijerumani kwa Marwa El Sherbini
Muuaji wa Marwa El-Sherbini, mwanamke wa Kimisri ambaye alichomwa visu mpaka kufa na muhamiaji mwenye asili ya Urusi na Ujerumani, Alex Wiens, ndani ya mahakama huko Ujerumani, amehukumiwa kifungo cha maisha, bila uwezekano wa kuachiwa mapema. Haki hatimaye imetolewa na muuaji anaadhibiwa, wanasema wanablogu wa Misri.
India: Usawa
“Takriban asilimia 15 ya watu ambao ni viongozi wa siasa na watumishi wa serikali, kwa kupitia vitendo vya kifisadi, wamejilimbikizia asilimia 85 ya utajiri wote wa India, na kuwaachia asilimia 15 tu ya utajiri huo asilimia 85 ya wananchi,” anasema Ram Bansal katika blogu ya India in Peril.
Palestina: Mtaa wa Twita
Eman katika AquaCool anatoa maoni kuhusu mtaa wa kwanza kupata jina linalotokana na huduma ya Twita, katika kambi ya wakambizi huko ukingo wa Magharibi.
Algeria-Misri: Ugomvi Juu ya pambano la Mpira kwenye Mtandao
Hali tete kati ya mashabiki wa mpira wa miguu wa Misri na Algeria inazidi kukua kabla ya pambano litakalofanyika mjini Cairo tarehe 14 Novemba. Mchuano huo utaamua ipi kati ya timu hizo zitafaulu kwenda kwenye Kombe la Dunia la FIFA Afrika ya kusini mwaka ujao. Misri inahitaji japo ushindi wa magoli mawili ili kulazimisha mchezo wa kukata shauri katika uwanja wa nchi nyingine ambapo Algeria, ambayo imeshindwa kufaulu kwenda kombe la dunia tangu 1986, itapambana ili kutunza nafasi yake ya sasa ya kuongoza katika kundi la wanaogombania nafasi ya kufaulu. Wakati wa kuelekea pambano la Jumamosi, mashabiki washindani wamekuwa wakijiandaa nje ya mtandao wa intaneti, kadhalika katika malumbano makali ya mtandaoni, ambayo yamekua na kugeuka “vita-vya-mikwara-kwenye-mtandao”
Syria: Simulizi Ya Ufukweni
Profesa wa Fasihi ya Kiingereza kutoka mji wa mdogo wa Tartous huko Mediterranean na mwandishi mwenye asili mchanganyiko ya Siria na Canada wakiwa safarini kuelekea kwenye nchi yake ya asili wanatizamana wakiwa kwenye mgahawa unaoitwa Sea breeze. Hivyo ndivyo Mariya na Abu Fares walivyoamua kuanza shani yao na kuwanasa kwa wasomaji wao. Yazan Badran anatupasha.
Jordan: Barua kwa MBC
M-jordan Ola Eliwat, kutoka Cinnamon Zone, anaandika barua ya wazi kwa makapuni ya televisheni ya MBC. Katika barua hiyo anaandika: “Na tafadhali fikirieni kufunga 90% ya idhaa zenu, nadhani itakuwa hisani KUBWA kwa taifa la Kiarabu!”
Uganda: Ugonjwa wa Panzi Waota Mizizi
Wanasiasa wa Uganda wanakuwa kama panzi: “kufuatia hali ya kufikia kikomo kwa tawala nyingi za kiimla, Museveni na washirika wake katika ukaliaji wa mabavu wa Buganda kwa kutumia silaha wanaanza kuwa kama panzi.”
Afrika Kusini: Wimbo wa Taifa kwa Wanaoongea Kiingereza
Wimbo wa Taifa wa Afrika Kusini kwa wanaoongea Kiingereza: Ni njia kuu iliyoje ya kufafanua kwa kuonyesha Wimbo wa taifa wa Afrika Kusini kwa wale kati yetu ambao kwanza hatuufahamu mpaka sasa, pili tunaoufahamu lakini pengine hatujui jinsi ya kutamka maneno yake na tatu ambao hatuongei lugha iliyo kwenye wimbo...
Naijeria: Wanablogu Wajadili Sifa Mbaya ya Naijeria
Inajulikana vyema kuwa Naijeria ina tatizo la muonekano – utapeli wa 419 kwenye intaneti, rushwa, uharamia wa mafuta katika jimbo la Delata – kwa watu wengi, huu ndio uhusiano unaokuja akilini wakati nchi yenye watu wengi zaidi Afrika inapotajwa.
Angola: Gharama za Juu za Maisha Mjini Luanda
Gharama kubwa ya maisha nchini haieleweki: viashiria vya maendeleo vya hali ya juu havishabihiani na hali ya kifedha ya Waangola wengi na havitafsiriki katika viwango vya maisha vya wasio na hali nzuri kiuchumi.