Habari kuhusu Myanmar (Burma)

Sinagogi Pekee Lililobaki Myanmar

  25 Februari 2014

Lilijengwa miaka 120 iliyopita, Sinagogi la Musmeah Yeshua lililoko eneo la Yangon ni Sinagogi pekee la wayahudi lililoyobaki katika eneo linaloongozwa na waumini wa dini ya Kibudha waishio nchini Myanmar. Mbali na kuwa kivutio cha utalii, pia limetajwa kama jengo la urithi la mambo ya kale katika mji huo.

PICHA: Maisha Nchini Myanmar

  4 Oktoba 2013

Mpiga picha Geoffrey Hiller ameweka kumbukumbu ya maisha yake nchini Myanmar kuanzia mwaka 1987 mpaka kipindi cha kihistoria kutokea nchini humo

Raia wa Myanmar Wachukizwa na Mashambulizi Dhidi ya Wahamiaji Wenzao Nchini Malasia.

  21 Juni 2013

Vurugu za kikabila nchini Mynmar inaonekana kusambaa hata katika nchi za jirani.. Baadhi ya wahamiaji wa Mynmar wa jamii ya budha wanaoishi nchini Malasia wiki chache zilizopita ambapo watu wengi wanaamini kuwa mashambulia hayo yanahusiana mvutano wa kimakabila na kidini unaoendelea nchini Myanmar. Mwitikio wa awali wa serikali ya Myanmar wa kukanusha matukio haya uliwakasirisha watumiaji wengi wa mtandao.

Uhuru wa Vyombo vya Habari Nchini Myanmar Bado ni Giza

  25 Februari 2013

Uamuzi wa Myanmar wa kuivunja bodi katili ya ukaguzi ilisifiwa na makundi mbalimbali ya watu kama njia ya kuelekea kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari nchini humo. Lakini, waangalizi wa uhuru wa vyombo vya habari waliainisha vitisho na mashambulio wanayokabiliana nayo waandishi wa habari wanaoishi nchini Myanmar.

Mkanganyiko wa Makubaliano ya OIC Kuanzisha Ofisi Nchini Myanmar

  30 Novemba 2012

Shirika la Ushirikiano wa Kiislam (OIC) limependekeza kuanzisha ofisi nchini Myanmar kwa lengo la kukisaidia kikundi kidogo cha Waislamu nchini humo. Serikali ilishakubaliana na mpango huu lakini ilibadili uamuzi huu mara baada ya kutokea maandamano ya kupinga uamuzi huo katika maeneo mengi ya nchi.

Mfumo wa Kipekee wa Kuwapa watoto Majina wa Nchini Myanmar (Burma).

  27 Agosti 2012

Raia wengi wa Myanmar hawana majina ya ukoo. Je, umewahi kujiuliza wanajaza vipi fomu zinazowadai kujaza majina yao ya mwanzo na ya ukoo, au hata kujiuliza kuwa 'Daw' ina maana gani katika jina la Daw Aung San Suu Kyi? Hapa tutatazama mtindo wa pekee kabisa wa Mynmar wa kutoa majina.

Makala za Global Voices Zilizosomwa Zaidi mwaka 2011

Global Voices haijabaki kuwa sauti pweke ya vyombo vya habari vya kiraia linapokuja suala la twita zinazotuma taarifa na posti za kwenye blogu. Bado, hata hivyo pale ambapo shauku kwa vyombo vikuu vya habari ikindelea kupungua, sisi ndio tunaojibidiisha kuendelea kuweka kumbukumbu ya kile ambacho wanablogu wadogo popote pale waliko wanahitaji dunia ikifahamu. Fahamu orodha ya makala zetu 20 zilizosomwa zaidi kwa mwaka 2011

Myanmar: Simulizi za Wafanyakazi wa Misaada Baada ya Tetemeko la Ardhi

  10 Aprili 2011

Myanmar bado inasumbuka kutokana na tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 6.8 ambalo liliikumba nchi hiyo. Mwandishi wetu aliyeko Myanmar anatafsiri mahojiano na simulizi za wakazi pamoja na wafanyakazi wa misaada ambao walishuhudia kiwango cha uharibifu uliofanywa na tetemeko hilo kaskazini mashariki mwa Myanmar.

Myanmar: Hatimaye Suu Kyi Amekuwa Huru

  20 Novemba 2010

Amekuwa kifungoni kwa miaka 15 katika miaka 21 iliyopita, lakini hivi sasa hatimaye yuko huru. Kiongozi wa upinzani na alama ya wapenda demokrasia nchini Burma, Aung San Suu Kyi aliachiwa huru kutoka kizuizini mchana siku ya Jumamosi na serikali inayoungwa mkono na jeshi la Myanmar

Asia ya Kusini Mashariki : Ngono na Udhibiti wa Mtandao

  26 Julai 2010

Uratibu wa maudhui katika intaneti unaonekana kana kwamba ni kinyume na demokrasia lakini serikali za Kusini Mashariki mwa Asia zinaweza kuhalalisha kitendo hicho kwa kuzusha haja ya kuwaokoa vijana kutoka kwenye janga la tabia za ngono holela.