Am a Kenyan citizen living in Nairobi. Graduated in tourism and currently working as a Tour Operator.
makala mpya zaidi zilizoandikwa na Joyce Maina kutoka Juni, 2013
Mwanaharakati wa Haki za Binadamu Nchini Saudi Afungwa Miaka Nane Jela
Abdulkareem al-Khadar, mwanafamilia ya kifalme mwanzilishi wa shirika la haki za binadamu, Chama cha ki-Saudi cha Haki za Kiraia na Kisiasa (ACPRA), alihukumiwa kifungo cha miaka nane jela kwa kosa la uchochezi na kuanzisha shirika la haki za binadamu lisilo na leseni pamoja na mashtaka mengine
Uzuri wa Mlima Everesti Nyakati za Usiku
Sinema fupi za Elia Saikaly zimenasa uzuri mkuu wa Mlima Everesti nyakati za usiku kwa kila sekunde. Anasimulia kwenye blogu yake uzoefu wake wa kupanda hadi kilele cha Mlima Everest kwa mara ya pili.
Athari za Mazingira kwa Uchimbaji Madini Nchini Indonesia
Makala iliyochapishwa katika mtandao wa mongabay.com imefichua athari za uharibifu wa kimazingira ziazotokana na shughuli za uchimbaji madini katika maeneo ya vijiji nchini Indonesia. Baadhi ya wanazuoni wanahofia kwamba maeneo mengi nchini Indonesia yana kiwango cha juu kabisa cha zebaki duniani.
Israeli: Waandamanaji Wakumbana na Ukatili wa Polisi Jijini Yerusalemu
Maandamano yaliyoandaliwa na vikundi vitatu vinavyohusiana na Vuguvugu la Israel la haki ya kijamii (#j14) yalifanyika jijini Yerusalemu mnamo Jumamosi usiku (Juni 8). Waandamanaji walidai kubatilishwa kwa uamuzi wa kuuza zaidi kiasi kikubwa cha hifadhi ya gesi wakati ni asilimia 12.5 tu ya mapato hayo yatakwenda serikalini kama kodi.
Bajeti ya Bangladesh: Maoni na Uchambuzi
“Bajeti ya kifahari lakini mpango duni?” Raia wa kawaida anatoa maoni na kuichambua bajeti ya hivi karibuni ya Bangladesh kwa mwaka wa fedha 2013-2014.
Misri Inavyopoteza Miji ya Kihistoria
Cairoobserver atoa wito [ar] kwa wakaazi wa Misri kupitia mtandao wa
Jamaica: Watoto kama Wasanii
Blogu ya Maonyesho ya Sanaa ya Taifa Nchini Jamaika inayo msisimko kuhusu maonyesho yajayo ya sanaa ya watoto, ambayo yataonyesha “mwitikio wa pekee wa watoto kwa maswali kuhusu udadisi wao na msukumo wa aina tofauti wa ubunifu unaokua.”
Misri: Wafanyakazi wa Asasi Zisizo za Kiserikali Nchini Misri Wafungwa Jela
Kuhukumiwa kwa wafanyakazi wa ki-Misri na kigeni wanaofanya kazi katika asasi zisizo za kiserikali (NGO) kifungo cha hadi miaka mitano jela, kumesababisha hasira katika mitandao ya kijamii na katika maeneo mengine. Hatua hiyo imeonekana kama onyo kwa mashirika ya kutetea haki za binadamu na yale yanayokuza demokrasia.
‘Sauti za Iran’ Mradi Unaowapa Sauti Raia Waishio Vijijini
Sauti za Iran ni mradi ulioundwa kwa kutumia mafanikio ya mradi wa Ushahidi. Sauti za Iran inakusudia kuripoti habari kuhusu miji midogo na vijiji vya Iran na vile vile kukusanya maombi na matatizo ya wananchi na kuyatuma kwa serikali na wabunge.
China Yadaiwa Kuchimba Dhahabu Kinyume cha Sheria Nchini Ghana
Shirika la Habari la Xinhua limeripoti kwamba raia 124 wa Kichina waliodaiwa kushiriki katika uchimbaji wa madini haramu ya dhahabu walikamatwa na kuwekwa kizuizini nchini Ghana. Serikali ya China imetakiwa kulinda na kuwatetea raia wake. Kwa upande mwingine, maoni yaliyotokana na tukio hilo yaliukosoa unyanyasaji unaofanywa dhidi ya watu wa Afrika katika biashara ya...