Am a Kenyan citizen living in Nairobi. Graduated in tourism and currently working as a Tour Operator.
makala mpya zaidi zilizoandikwa na Joyce Maina kutoka Agosti, 2012
Tanzania/Malawi: Utafutaji Mafuta kwenye Ziwa Nyasa WachocheaMgogoro wa Umiliki
Taarifa kwamba Malawi inatafiti mafuta katika Ziwa Nyasa (linalojulilkana pia kama Ziwa Malawi) zimeibua mjadala motomoto. Wakati ambapo serikali ya Malawi inadai umiliki kamili wa ziwa hilo, Tanzania inataka mpaka utambuliwe kuwa katikati ya ziwa.
Ufilipino: Mafuriko Yaathiri Vitongoji vya Jiji la Manila na Mikoa ya Karibu
Mvua kubwa ilisababisha mafuriko katika vitongoji vingi ya jiji la Manila pamoja na majimbo ya jirani katika Kisiwa cha Luzon nchini Ufilipino. Mhariri wa Global Voices aliye huko Manila, Mong Palatino, anakusanya picha kutoka katika majukwaa mbalimbali ya habari za kiraia yanayoonyesha athari kubwa ya mafuriko hayo katika mji huo mkuu wa nchi.
Mauritania: Wafanyakazi wa Migodini Wapinga ‘Aina Mpya ya Utumwa’
Zaidi ya wafanyakazi 2,300 wako kwenye mgomo nchini Mauritania katika mji wa kaskazini wa Zouerat, jambo ambalo limesababisha kuzorota kwa maeneo mengine kumi ya Kampuni la Taifa la Madini na Viwanda, huku kazi zikiwa kwenye mvurugiko mkubwa. Madai yamejikita katika suala zima la maslahi bora ya wafanyakazi.
Saudi Arabia: Mwanaharakati Reema Al Joresh Atiwa Kizuizini katika Sikukuu ya Idi
"Hamjambo? Polisi wamenikamata mimi na watoto wangu." - Reema Al Joresh, mke wa mfungwa ambaye amekuwa kizuizini kwa miaka nane bila kufunguliwa mashtaka, alikuwa akielekea msikitini ili kutoa zawazi 500 pamoja na barua ya kueneza taarifa kuhusu itiaji nguvuni wa kiholela katika ufalme huo.
Morocco: Wanafunzi Wadai Marekebisho kwenye Mfumo wa Elimu
Mwezi Julai, kikundi cha wanafunzi wa nchini Morocco kilizindua ukurasa wa Facebook ulioitwa "Umoja wa Wanafunzi wa Morocco kwa ajili ya Mabadiliko ya Mfumo wa Elimu". Pungufu ya mwezi mmoja, kikundi hiki kilivuta uungwaji mkono mkubwa hasa kupitia mitandao ya kijamii.