Am a Kenyan citizen living in Nairobi. Graduated in tourism and currently working as a Tour Operator.
makala mpya zaidi zilizoandikwa na Joyce Maina kutoka Julai, 2012
Basi la Watalii Raia wa Israeli Lashambuliwa Nchini Bulgaria
Watu wapatao saba wameuawa katika shambulio la la kijana wa Kiyahudi katika basi la kitalii lililokuwa katika uwanja wa ndege wa Burgus nchini Bulgaria. Ripoti zinadai shambulio linaonekana kuwa la kujitolea mhanga, lililofanywa na kijana alikuwa ama karibu na basi au alikuwa ndani ya basi.
Tamko la Uhuru wa Mtandao wa Intaneti
Hivi karibuni, makundi kadhaa yameungana pamoja kutengeneza Tamko la Uhuru wa Mtandaoni. Mpaka sasa, Tamko hilo limesainiwa na mashirika na kampuni zipatazo 1300 na bado zoezi linaendelea kukua.
Ethiopia: Maandamano ya Waislamu Yashika Kasi
Jeshi la Polisi nchini Ethiopia waliamua kutumia nguvu kupambana na wanaharakati wa ki-Islamu, likituhumiwa kufanya vitendo haramu katika maeneo yanayochukuliwa kuwa matakatifu katika misikiti, kwa mujibu wa habari zilizoandikwa na ukurasa wa kikundi cha waislam katika mtandao wa Facebook uitwao Dimtsachin Yisema (Iache Sauti Yetu Isikike). Tangu mwezi Mei, Wa-Islamu wa ki-Ethiopia wamekuwa wakiandamana kupinga serikali kuingilia mambo yao ya kidini.
Palestina: Makala Kuhusu Kifo cha Arafat yaibua maswali
Kituo cha habari cha Al Jazeera hivi karibuni kilionyesha makala iliyohusu kifo cha utata cha rais wa Palestina Yasser Arafat kilichotokea mjini Paris mnamo Novemba, 2004. Makala hayo yanadai kwamba kiongozi huyo hakufa kifo cha kawaida, ila aliwekewa sumu ya poloni, madai ambayo yanaibua maswali mengi.